• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC SONGWE AITAKA BODI YA MAJI KUSIMAMIA VEMA UPATIKANAJI WA MAJI.

Posted on: March 5th, 2018

  Mkuu wa Mkoa wa Songwe Chiku Gallawa ameitaka Bodi Mpya ya Mamlaka ya Maji ya Vwawa-Mlowo aliyoizindua mapema leo, kusimamia upatikanaji wa maji safi na salama Mkoani hapa.

Gallawa ametoa rai hiyo nakuitaka bodi hiyo kuwa msimamizi wa huduma za maji huku akiitaka ijikite katika kubuni mbinu mbalimbali za kuboresha upatikanaji wa maji na utoaji wa huduma za maji kwa ufanisi.

“Bodi hii kwanza itusaidie kuongeza asilimia ya upatikanaji wa maji angalau tufikie asilimia 90 ifikapo mwaka 2020, pili ishirikiane na wadau kubuni mbinu mbalimbali za kuboresha huduma ya maji, lakini pia isimamie utunzaji wa vyanzo vya maji”, amesisitiza Gallawa.

Ameongeza kuwa bodi hiyo ijiendeshe kidijitali kwa kuweka mfumo wa kutuma bili za maji kwa mfumo wa ujumbe mfupi na kusisitiza kuwa wateja wawekewe mita na bili zao ziwe halisi sawasawa na matumizi yao.

Gallawa amesema, “Tumepiga vita biashara ya mkaa ili kutunza mazingira, bodi ihakikishe sasa vyanzo vyote vya maji vinalindwa pia iweke mikakati ya uvunaji wa maji ya mvua kwa mabwawa na hata kwa majumbani na pia mkakati mwingine uwe wa kuhakikisha maji yanayopatikana yanakuwa safi na salama”.

Amewahakikishia wajumbe kuwa ana imani na utendaji wao huku akiwataka kushirikiana na halmashauri katika kuthibiti taka ngumu kwakuwa zinaweza kuchafua vyanzo vya maji hivyo kuleta magonjwa ya mlipuko.

Aidha amewatahadharisha kusimamia vema mapato yatakayokusanywa, fedha za wadau na fedha kutoka serikalini ili mamlaka iweze kusimama imara pia wasimamie miradi ya maji inayojengwa ikamilike kwa muda na kwa ubora unaotakiwa.

Naye Mwenyekiti wa Bodi hiyo Asanga Malalwale Ndile ameshukuru Mkuu wa Mkoa wa Kuzindua bodi hiyo pamoja ushirikiano ambao amekuwa akiwapatia wakat wa uundwaji wake.

Ndile amesema atahakikisha anashirikiana na wajumbe, wadau na serikali katika kuhakikisha sekta ya maji Mkoa wa Songwe inaboreshwa huku akiwa na imani kuwa bodi hiyo itafanya vizuri kiutendaji licha ya upya wake.

Kwa upande wake Mhandisi wa Maji Mkoa wa Songwe Tanu Deule ameeleza kuwa hali ya upatikanaji wa maji kwa Mkoa wa Songwe ni asilimia 42.5 ambapo matarajio ni kuwa ifikapo Juni 2018 hali ya upatikanaji wa maji itakuwa ni asilimia 59.61.

Deuli ameongeza kuwa asilimia hiyo ya maji itaongezeka mara tu baada ya kukamilika kwa miradi zaidi ya kumi ya maji iliyopo kwenye bajeti ya mwaka 2017/18.

Mhandisi wa Maji Mkoa wa Songwe Tanu Deule akisoma taarifa ya hali ya upatikanaji wa maji wakati wa uzinduzi wa bodi ya Mamlaka ya Maji ya Vwawa-Mlowo.


Matangazo

  • ILEJE DC WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2021 December 18, 2020
  • MBOZI DC WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2021 December 18, 2020
  • MOMBA DC WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2021 December 18, 2020
  • SONGWE DC WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2021 December 18, 2020
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Dkt. SHEKALAGHE VYUO VYA UFUNDI NA VIKUNDI VYA UJASILIAMALI MBADALA KWA WANAFUNZI AMBAO HAWAJAFAULU

    December 18, 2020
  • Dkt. SHEKALAGHE AZITAKA HALMASHAURI KUTENGA PESA YA UJENZI WA MADARASA KILA MWAKA.

    December 18, 2020
  • SONGWE: WANANCHI WAHIMIZWA KUPIMA UKIMWI KUJUA HALI ZAO KUEPUKA MAAMBUKIZI MAPYA

    December 01, 2020
  • RC MWANGELA AWATAKA WAFANYABIASHARA KUUZA BIDHAA KWA BEI ELEKEZI

    November 28, 2020
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Boma Road, Vwawa, Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras.songwe@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.