• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

BILIONI 20.9 KUBORESHA BARABARA, MADARAJA

Posted on: September 9th, 2022

BILIONI 20.9 KUBORESHA BARABARA, MADARAJA

Na. Nicholas Ndabila

SONGWE: Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) katika bajeti ya 2022/2023 imetenga fedha Bilioni 20.9 kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya Barabara yenye urefu wa Kilomita 3341.1 pamoja na madaraja.

Hayo yamesemwa na Meneja wa TARURA Mkoa wa Songwe Eng. Kilian Daudi Haule Katika hafla ya utiaji saini mikataba mitano kati ya TARURA na Makandarasi iliyosainiwa Septemba 9 na kushuhudiwa na Mkuu wa Mkoa wa Songwe pamoja na wakuu wa Wilaya katika ukumbi wa Mkoani.

Kampuni zilizo saini mikataba hiyo ni Kampuni ya Lusubilo Wandarasi iliyo saini mkataba waenye thamani ya Shilingi Million 56.3, HANSAF Company Limited iliyoko wilayani Ileje Mkataba wenye thamani ya Shilingi Millioni 210.1, DAR Form company Limited iliyoko wilaya Mbozi mkataba wenye thamani ya shilingi Millioni 312.37, Rwechotes Company Limited inayopatikana halmashauri ya Tunduma imesaini mkataba wenye thamani ya Shilingi Millioni 168.5 pamoja na kampuni ya GNMS Contructors Company Limited iliyoko wilaya ya Songwe iliyo saini mkataba wenye thamani ya shilingi Million 598.878.

Mkuu wa Mkoa wa Songwe Mhe. Waziri Kindanba ameishukuru sana Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwajali wananchi kupitia kutekeleza miradi mbali mbali ndani na nje ya mkoa wa Songwe.

Amewataka wakandarasi kutekeleza wajibu wao na kuwa waadirifu kufanya kazi bora na kukamilisha miradi hiyo kwa wakati lakini pia amewasihi Uongozi wa TARURA wilaya na Mkoa kusimamia miradi hiyo kwa ukaribu na ubora kutokana na masharti ya mikataba iliyo sainiwa.

"Kama jambo hulifuatilii na kulisimamia kwa ukaribu litafanywa chini ya kiwango lazima ukague lazima uende eneo la kazi uangalie nini kinafanyika" Mhe. Waziri Kindamba Mkuu wa Mkoa wa Songwe.

Mwenyekiti CCM Mkoa wa Songwe Ndug. Elynico Mkola amemshukuru Rais wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutekeleza Ilani Chama Cha Mapinduzi kwa vitendo kwa kutekeleza miradi mbalimbali ya huduma za afya na jamii.

Fungo Atukuzwe Alex mkandarasi wa kampuni ya HANSAF CO. Limited inayo patikana Wilaya ya Ileje ameishukuru Serikali kwa kuwaamini na kuahidi kuitekeleza miradi kwa wakati na kwa weledi kwa hali ya juu kama walivyo ingia makubaliano na Serikali katika mkataba uliosainiwa.

MWISHO.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.