• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

HUDUMA ZA AFYA ZAIMARIKA ZAIDI TUNDUMA.

Posted on: October 7th, 2022

HUDUMA ZA AFYA ZAIMARIKA ZAIDI TUNDUMA.

 

TUNDUMA: Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluh Hassan imezidi kuboresha huduma za Afya katika Halmashauri ya Mji Tunduma kwa kuongeza zaidi vifaa tiba, watalamu wa Afya pamoja na kuboresha miundombinu ya huduma za Afya.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Wilaya ya Momba, Mhe. Fakii Lulandala wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Waziri Kindamba ya ukaguzi wa miradi katika Halmashauri ya Mji Tunduma, Oktoba 7 akiwa katika Hospitali ya Mji wa Tunduma.

Mhe. Fakii Lulandala amesema ujenzi wa vituo vya Afya vya, Chapwa, Chiwezi, Chipaka na Mwaka kati pamoja ujenzi wa hospitali ya Halmashauri ya Mji Tunduma unaonyesha ni jinsi gani Mhe. Samia Suluh Hassan ana nia nzuri ya kuboresha nazingira ya utoaji huduma za afya kwa wananchi wa Tunduma na Wilaya ya Momba.

Mganga mfawidhi wa Hospitali ya Halmashauri ya Mji Tunduma, Dkt. Aboubakari Mfaume amesema kitendo cha Serikali ya awamu ya sita kuongeza watumishi wa Afya, kuleta vifaa tiba kama X-ray inasaidie kuimarisha utoaji wa huduma za Afya katika Hospitali ya Tunduma.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Tunduma, Bwn. Philemon Magesa amesema tayari Serikali ya awamu ya sita imeleta fedha milioni 376 za ukamilishaji wa jengo la OPD katika Hospitali hiyo.

Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Waziri Kindamba ameupongeza uongozi wa Halmashauri ya Mji Tunduma kwa kuamua kuanza kutoa huduma katika Hospitali hiyo, kwani hii ndio maana halisi ya Kazi iendelee.

Aidha, Mkuu wa Mkoa amesisitiza watumishi wa Afya watumie lugha nzuri pale wanapotoa huduma kwa wananchi, Mhe. Kindamba amesema eneo la Afya ni eneo ambalo likikosa huduma bora kwa wananchi linaweza kuzalisha kero nyingi kwa wananchi.

Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa, Mhe. Waziri Kindamba amewapongeza viongozi wa Tunduma kwa kufanya kazi kwa kushirikiana katika kuleta maendeleo kwa wananchi na kuwataka waepuka migogoro ambayo inaweza kuwakwamisha.

MWISHO.

 

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.