• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

INDONESIA KUSHUSHA NEEMA MKOA WA SONGWE

Posted on: April 29th, 2021

Serikali ya Indonesia imekiri kuvutiwa na fursa za uwekezaji zilizopo katika Mkoa wa Songwe, hususani kwenye sekta za kilimo, Madini, Biashara na Bandari kavu, ambapo imeonyesha nia ya kutaka kuwekeza katika maeneo hayo.

Balozi wa Indonesia Nchini  Profesa Ratlan Pardede amebainisha leo Mei 29 katika ziara yake ya siku mbili mkoani hapa kwa lengo la kutembelea na kujionea fursa za uwekezaji zitakazowezesha kupatikana manufaa ya kiuchumi kati ya Tanzania na Indonesia kupitia Mkoa wa Songwe.

Profesa Pardede ambaye pia ni mwakilishi wa nchi hiyo katika nchi za Burundi, Rwanda na Comoro, alitaja miradi na maeneo ambayo wao wameyaona kama fursa ya uwekezaji kuwa ni eneo la kilimo, ambapo nchi hiyo itawezesha ujenzi wa viwanda vya kuchakata chakula cha mifugo.

"Kama mlivyoonyesha katika taarifa yenu iliyowasilishwa hapa leo kuhusu kilimo, katika eneo hili tumebaini kuna fursa kubwa ya uwekezaji wa viwanda vya kuchakata chakula cha mifugo ili kuongeza tija kwa wakulima.", amesema Profesa Pardede.

Ametaja maeneo mengine kuwa ni mpaka wa Tunduma kati ya Tanzania na Zambia ambao ni lango la nchi za Jumuiya ya Maendeleo kusini mwa Afrika(SADC) kuwa kuna fursa kubwa ya biashara, ambapo wanalenga kufungua maduka makubwa (Shoping Mall) ambayo yatakuwa na bidhaa za indonesia ikiwa ni pamoja na ujenzi wa bandari kavu.

Katibu Tawala Mkoa wa Songwe Dkt. Seif Shekalaghe aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa amesema ziara hiyo imekuwa na mafanikio makubwa kwa mkoa wa Songwe ambao ni mzalishaji mkubwa wa mazao ya chakula.

"Tumeona fursa ya wakulima wetu kufanya biashara ya kuuza maparachichi ambayo yanazalishwa kwa wingi hapa kwetu, lakini pia zao la soya ambalo soko lake ni kubwa katika nchi ya Indonesia.", Amesema Dkt. Shekalaghe.

Kwa upande wake, Mwenyekiti waWenye Viwanda, wafanyabiashara na wakulima (TCCIA) Songwe Mkoa wa Songwe, Charles Chenza amesema wanatarajia kutumia fursa hiyo ya ushirikiano wa nchi hizi mbili katika kuimarisha biashara ya bidhaa za kilimo.

Balozi Profesa Pardede ameongozana na Naibu Balozi wa nchi hiyo, Wahono Yulianto, pamoja Ofisa wa mambo ya nje kutoka Wizara ya Mambo ya Nje, Luangisa Emmanuel ambao wamefanikiwa kutembelea Wilaya za Ileje, Mbozi na Halmashauri ya Mji Tunduma.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.