• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

JITIHADA ZAIDI ZINAHITAJIKA KUONGEZA UFAULU KIDATO CHA SITA.SONGWE:

Posted on: July 8th, 2022

JITIHADA ZAIDI ZINAHITAJIKA KUONGEZA UFAULU KIDATO CHA SITA.SONGWE:  

Waratibu elimu kata amewatakiwa kuongeza jitihada zaidi katika usimamizi wa shule ili kuongeza ufaulu wa wanafunzi wa kidato cha sita.

Wito huo umetolewa na Kaimu  Katibu Tawala Mkoa, Ndg. Steven Pankras wakati akifungua kikao kazi cha waratibu elimu Kata, Maafisa elimu, wathibiti ubora wa Shule,  pamoja na tume ya utumishi wa waalimu kilichofanyika Julai 8 ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

Ndg. Pankras amesema licha ya waalimu kujitahidi kuondoa daraja la sifuri kwa kidato cha sita lakini bado mkoa haujafanya vizuri  ukilinganisha na idadi ya wanafunzi waliopo kwa kidato cha sita.

"Miaka ya nyuma miundombinu ndio ilikuwa kikwazo kwa wanafunzi kufaulu lakini saizi Serikali ya awamu ya sita imejitahidi kuboresha miundombinu ya shuleni hivyo kazi imebaki kwetu waalimu, tuongoze bidii kwa hili" amesema  Pankras.

Mwaka huu Wanafunzi wapatao 1,353 katika shule 18 wamefanya mtihani wa kuhitimi kidato cha sita katika matokeo Yao waliopata daraja la kwanza walikuwa 351, daraja la pili 773, daraja la tatu 205 na daraja la nne ni 1 huku daraja la sifuri hakuna wanafunzi aliyepata.

"Unakuta shule ina wanafunzi 12 au 7 lakini inashindwa kutoa daraja la kwanza kwa wanafunzi wote hii haijakaa vizuri kabisa" amesema Pankras.

Aidha, Ndg. Pankras amesema lengo la Mkoa wa Songwe ni kuona shule zinafanya vizuri kwa kuongeza daraja la kwanza na la pili,  amewataka viongozi wa elimu kuanzia ngazi ya Kata hadi Mkoa kutofurahia kuondoa daraja sifuri tu bali waongeze kasi ya kuapata daraja la pili na la kwanza  ili wanafunzi wapate fursa ya kujiunga na vyuo vikuu mbalimbali.

Afisa Elimu Mkoa wa Songwe, Mwl. Michael Ligola amesema lengo la kikao hicho ni kujadili matokeo ya mtihani wa upimaji wa Kanda wa darasa la saba, kutoa mrejesho wa kikao cha maafisa elimu wa Mkoa kilichofanyika mkoani Tabora na  kuweka mikakati bora ya kuongeza ufaulu wa elimu kuanzia msingi hadi kidato cha sita pamoja na kuboresha usimamizi wa miradi.

Afisa elimu msingi Halmashauri ya Mji Tunduma, Mwl. Wilson Mtafya akiongea kwa niaba ya wajumbe wa kikao hicho amesema watakwenda kufanyia kazi mapungufu yote yaliyojitokeza ili kuongeza ufaulu kwani kitendo cha mwanafunzi kushindwa kufanya vizuri kidato cha sita kunapelekea malengo yake kutotimia ya kwenda vyuo mbalimbali.

Ndg. Pankras amezitaka Shule binafsi ziwe chachu ya kuongeza daraja la kwanza  kwa kuwa wazazi/walezi wanatoa ada na shule nyingi zina idadi ndogo ya wanafunzi ukilinganisha na za Serikali hivyo tunatarajia makubwa kutoka kwao wakati na za Serikali nazo zinategemewa zifanye makubwa ndani ya Mkoa.

Wakati huo huo, Ndg. Stephen Pankras ametoa wito kwa waalimu kuwajengea uwezo wa kipekee kwa watoto ambao hawajui kusoma, Kuandika na Kuhesabu ili kusitokee mtoto anafika darasa la saba au la nne hajui kusoma, Kuandika na Kuhesabu.

MWISHO.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.