• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

KAFULILA KUWASHUGHULIKIA WATOA TAKWIMU ZA UONGO

Posted on: November 22nd, 2018

  Katibu Tawala Mkoa wa Songwe David Kafulila ameahidi huwashughulikia watumishi wanaotoa takwimu za uongo kwakuwa zimekuwa zikikwamisha mipango mbalimbali ya maendeleo.

Kafulila ameyasema hayo wakati akifungua mafunzo ya awali ya mipango na bajeti ya masuala ya lishe ngazi ya mkoa na halmashauri yaliyofanyika katika ukumbi wa halmashauri ya Wilaya ya Mbozi mapema wiki hii.

“Watendaji wa halmashauri mmekuwa mkitoa takwimu ambazo sio sahihi jambo ambalo linaathiri mipango mbalimbali, Sitaweza kusita kumchukulia hatua mtumishi yeyote ambaye atafanya makosa hayo na ninaelekeza watendaji ngazi ya mkoa msipokee tu taarifa bila ya kuzihakiki”, amesisitiza.

Aidha Kafulila amewashukuru wadau wa maendeleo akitoa mfano wa shirika la UNICEF ambalo limekuwa likisaidia masuala ya Afya na Lishe na kuongeza kuwa juhudi za wadau hawa hazitafanikiwa endapo takwimu watakazopewa zitakuwa sio sahihi.

Amezielekeza halmashauri kutenga fedha kwa ajili ya shughuli za lishe kama miongozo inavyosema na kutoa fedha zikatekeleze mipango iliyowekwa huku akimtaka afisa anayesimamia bajeti ngazi ya Mkoa kusimamia utekelezaji wa maelekezo hayo.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt Kheri Kagya amesema wastani wa watoto 37 kati ya 100 mkoani Songwe wamedumaa ikiwa ni kiwango kikubwa kuliko wastani wa kitaifa wa watoto 34 kati ya 100.

Dkt Kagya ameongeza kwa kuwashukuru UNICEF wanaofadhili utafiti wa hali ya lishe kwa mkoa wa Songwe, utafiti ulioanza Septemba 2018 na unatarajiwa kukamilika Januari 2019.

Amesema matokeo ya  awali ya utafiti huo bado yanaonyesha kuwa hali ya udumavu Mkoani Songwe si nzuri hivyo halmashauri zifuate maelekezo ya Katibu Tawala Mkoa ya kutenga na kutoa fedha kwa ajili ya masuala ya lishe.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.