• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

KILIMO CHA MBOGAMBOGA, MITI YA MATUMDA CHAHIMIZWA SHULENI.

Posted on: September 22nd, 2022

KILIMO CHA MBOGAMBOGA, MITI YA MATUMDA CHAHIMIZWA SHULENI.

SONGWE: Wajumbe wa Kamati ya lishe Mkoa wa Songwe, wameazimia kila Shule ya msingi na Sekondari kuanza kupanda Bustani za mbogamboga na matunda Ili kuboresha lishe kwa watoto.

Kamati ya Mkoa imetoa wito huo wakati wa kikao cha robo cha lishe cha kupitia utekelezaji wa Afua za lishe kilichofanyika 22 Septemba 2022.

Mjumbe wa Kamati hiyo Charles Chenza amesema kamati iweke azimio la kuitaka kila shule ipande miti ya matunda kama maparachichi, maembe kulingana na hali ya hewa ya shule ni tunda lipi linakubali pamoja na Bustani ya mbogamboga kwa ajili ya lishe kwa wanafunzi.

Naye mwakilishi wa Kamati ya Amani Mch. Rogers Simkonda amesema jamii imekuwa ikipuuza suala la kulima mazao na bustani majumbani mwao na hata kwenye taasisi kama mashule na kuacha maeneo wazi.

"Kwenye taasisi zetu kama mashule hakuna jitihada za kuzalisha chakula kwa ajili ya chakula cha mchana lakini hayo hayafanyiki na hata mazao kama migomba iliyopandwa kwenye maeneo hayo imeanza kuharibika na hakuna ufuatiliaji" amesema Simkonda.

Kwa upande wake Katibu Tawala Mkoa wa Songwe, Bi. Happiness Seneda amesema licha ya Mkoa wa Songwe kuwa moja ya mikoa inayozalisha chakula kwa wingi lakini ni miongoni mwa mikoa inayokabiliwa na udumavu unaosababishwa na lishe isiyozingatia ubora.

"Ukosefu wa lishe bora kwa Mtoto ni hatari kwa maisha yake na jamii, hivyo tujitahidi siku 1,000 za mwanzo tuimarishe lishe ikiwemo kuhakikisha mama mjamzito anapata lishe bora na mtoto naye" Bi. Happiness Seneda.

Amesema kuanzia sasa ulimaji wa Bustani na upandaji wa miti ya matunda upewe kipaumbele na kumjengea mtoto tabia ya kulima mbogamboga na matunda tangu akiwa shuleni.

MWISHO.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC CHONGOLO AONGOZA KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI WILAYA YA MOMBA KUJADILI HOJA ZA CAG

    June 11, 2025
  • RC CHONGOLO AONGOZA KIKAO CHA KUJADILI HOJA ZILIZO BAINISHWA KATIKA RIPOTI YA CAG HALMASHAURI YA MBOZI

    June 10, 2025
  • RC CHONGOLO APIONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA ILEJE KWA KUPATA HATI SAFI

    June 10, 2025
  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.