• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

KIMONDO CHA MBOZI KUTUMIKA KUTANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI SONGWE

Posted on: June 25th, 2018

  Serikali Mkoani Songwe imedhamiria kutangaza fursa za uwekezaji katika sekta mbalimbali ikiwemo utalii kupitia maadhimisho ya siku ya Kimondo Duniani Juni, 30 yatakayofanyika kwa mara ya kwanza nchini.

Mkuu wa Mkoa wa Songwe Chiku Gallawa amesema maadhimisho haya yatakayofanyika katika eneo kilipo kimondo cha Mbozi na matarajio ni kuwa yatavutia watalii na wawekezaji kutoka ndani na Nje ya nchi.

Ameongeza kuwa Mkoa wa Songwe unazo fursa za uwekezaji katika utalii, viwanda, kilimo, madini na biashara hivyo wawekezaji wazawa na hata wale wa nje ya nchi wanakaribishwa kuwekeza.

“Maadhimisho haya yatafanyika kwa muda wa siku tatu, tarehe 28 Juni tutakuwa na fainali za mpira wa pete na miguu, tarehe 29 Juni tutakuwa na kongamano la kitaaluma na uwekezaji na tarehe 30 Juni ndio kilele cha maadhimisho ya siku ya kimondo Dunia, tutatoa zawadi kwa washindi mbalimbali na tunarajia kuwa na watu zaidi ya elfu hamsini,” amesema Gallawa.

Aidha Kila halmashauri mkoani Songwe imepewa eneo katika kijiji cha Ndolezi kilipo Kimondo kwa ajili ya kutangaza fursa za uwekezaji, huduma na bidhaa wanazozalisha pamoja na taasisi na Wizara ya Maliasili na Utalii watakuwa na eneo la kutangaza fursa za uwekezaji na utalii nchini.

Gallawa ameongeza kuwa Mkoa wa Songwe unayo maeneo mengi ya utalii ikiwemo eneo lenye majimoto katika Kijiji cha Nanyara, unyayo wa Binadamu wa kale, hifadhi ya wanyamapori ya Piti/Lukwati na maporomoko ya maji.

Kimondo cha Mbozi chenye uzito wa tani 16 ni cha kwanza kwa ukubwa nchini Tanzania, cha pili Afrika na cha nane kwa ukubwa duniani kikiwa na sifa ya pekee ya kuwa na madini ya chuma kwa asilimia 90 hivyo kuwa cha baridi muda wote hata wakati wa jua kali.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.