• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

KITENGO CHA MANUNUZI CHAKWAMISHA MANUNUZI KWA MIEZI 3 MRADI WASUA SUA, RC MGUMBA ATOA MAELEZO.TUNDUMA

Posted on: June 8th, 2022

KITENGO CHA MANUNUZI CHAKWAMISHA MANUNUZI KWA MIEZI 3 MRADI WASUA SUA, RC MGUMBA ATOA MAELEZO.TUNDUMA: 

Manunuzi ya bidhaa mbalimbali za ujenzi wa Kituo cha Afya mwaka kati yamekwama kwa takribani miezi 3 katika kitengo cha manunuzi hali iliyopelekea mradi kwenda kwa kusua sua.Hayo yameibuka tarehe 7 Juni wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Omary Mgumba alipofanya ziara ya kukagua mradi wa kituo cha Afya mwaka kati na kukuta moja ya changamoto iliyopelekea mradi kusua sua ni kutokana na mtumishi wa Kitengo cha manunuzi kukaa na madokezo ya manunuzi ya kituo hicho kwa takribani miezi 3 bila kufanya manunuzi.Katibu tawala wilaya ya Momba, Bi. Mary Marcus amesema wasimamizi wa mradi wamefanya malipo ya milioni 16 kununua saruji lakini hadi sasa hawajapata ata mfuko mmoja wa saruji wa kujengea hali iliyopelkea kuuazima saruji ndio ujenzi ukaanza.Kaimu mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Mji wa Tunduma, Ndg. Josephat Kayombo Amesema mtumishi huyo aliyekaa na madokezo kwa miezi 3 amesimamishwa kazi tayari tangu Aprili 2022 kwa kosa la kuchelewesha ukamilishaji wa miradi baada ya kuona amekuwa kikwazo kwenye miradi mbalimbali ambayo inaendelea kutekelezwa.Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Omary Mgumba amewataka watalamu wa manunuzi kufahamu sio kila fedha inayokuja lazima wapate, kuna mengine yanafanyika kwa sababu ya mishahara inayolipwa.“Kweli tunakubali kila mbuzi anakula kwa urefu wa kamba yake lakini afisa uyu wa manunuzi kwa kukaa na madokezo miezi 3 yeye ameamua kukata na kamba yake kabisa” Mhe. Omary Mgumba.Mtumishi kama huyu sio wa kumsimamisha kazi tu anapaswa kutumia fedha zake kukamilisha mradi kama ikithibitishwa amefanya ubadhilifu kwenye mradi, amesema Mhe. Omary Mgumba.Mkuu wa Mkoa amesema pamoja na changamoto izo ambazo zimejitokeza swala la kukabidhi mradi wa kituo cha Afya ifikapo Juni 30 uko pale pale watalamu wafanye kazi usiku na mchana.Serikali kuu imeleta fedha milioni 500 fedha za tozo za miamala ujenzi wa kituo cha Afya mwaka kati ambacho kinakwenda kuwaondolea usumbufu wananchi kusafiri umbali wa zaidi KM 8 kufuata huduma.Wakati huo huo Mkuu wa Mkoa amewataka watumishi kuacha tabia ya kulindana pale wanapoona kuna mwenzao anaaribu kazi kwa maslahi ya Taifa.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.