• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MAANDALIZI YA KUKABILIANA NA CORONA YAFIKIA HATUA NZURI

Posted on: March 26th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brig. Jen. Nicodemus Mwangela ameibanisha Kuwa maandalizi ya kukabiliana na Ugonjwa wa Virusi vya Corona kwa Mkoa wa Songwe yapo vizuri huku akizielekeza Halmashauri za Wilaya kukamilisha baadhi ya mapungufu yaliyopo.

Brig. Jen. Mwangela ameyasema hayo jana akiwa na Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa mara baada ya kukamilisha ukaguzi wa utayari wa kukabiliana na Ugonjwa wa Virusi vya Corona katika Halmashauri  za Mbozi, Ileje na Halmashauri ya Mji Tunduma.

Amesema watalaamu wa Afya ambao watawahudumia wagonjwa wa Corona endapo watatokea Mkoani Songwe tayari wana mafunzo na Uelewa wa majukumu yao huku Vituo vilivyo teuliwa kwa ajili ya kuhudumia wagonjwa na washukiwa vimezingatia maelekezo ya Wizara ya Afya.

Brig. Jen. Mwangela ameongeza kuwa amebaini baadhi ya vituo vya kutolea huduma kwa wagonjwa na Washukiwa wa Corona vina mapungufu kadhaa ikiwemo uhaba wa maji, umeme na baadhi ya vifaa tiba na kinga ambapo ameziagiza Halmashauri husika kukamilisha mahitaji hayo haraka sana.

Wakati huo huo Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brig. Jen. Nicodemus Mwangela ametoa elimu ya Kujikinga na Virusi vya Corona kwa wasafiri, madereva na wafanyakazi wengine wa Mabasi katika maeneo mbalimbali huku akiwasisitiza kuchukua hatua za tahadhari kwa kunawa mikono na kuepuka mikusanyiko isiyo ya Lazima.

Naye Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi wa Polisi George Salala amewaagiza wamiliki wa vyombo vya usafiri kuhakikisha hawajazi abiria kuliko uwezo wa gari kwakuwa ni kutengeneza mkusanyiko usio wa lazima huku akisema hatua kali zitachukuliwa kwa watako kaidi.

Kamishna Msaidizi wa Polisi Salala ametoa angalizo kwa abiria pia kutokubali kupanda mabasi au usafiri endapo watakuta umejaa kwani mikusanyiko kama hiyo ni mojawapo ya njia ya kusambaza ugonjwa wa Virusi vya Corona.

Amesema wamiliki wa mabasi wanapaswa kuweka maji ya kunawa yenye dawa katika mabasi yao ili kuwakinga madereva wao na kuwakinga abiria dhidi ya Ugonjwa wa Virusi vya Corona kwakuwa ili kufanikisha kutosambaa kwa ugonjwa huo inatakiwa jamii yote ishirikiane.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Songwe Dkt Hamad Nyembea amesema mpaka sasa maandalizi ya Utayari wa kukabiliana na Ugonjwa wa Corona kwa Mkoa wa Songwe yamefikia asilimia 50 huku mapungufu yaliyobainishwa yatakamilishwa ifikapo mwishoni mwa wiki hii.

Dkt Nyembea ameongeza kuwa kufuatia agizo la Serikali la kuwaweka karantini siku 14 watu wote walio toka nchi zenye maambukizi Zaidi ya Virusi vya Corona hadi sasa wamewaweka watu sita karantini waliotumia mpaka wa Tunduma kutokea nchi ya Afrika Kusini.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.