• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MAKAMU WA RAIS KUFANYA ZIARA YA SIKU TANO YA KIKAZI MKOANI SONGWE

Posted on: July 17th, 2018

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kufanya ziara ya siku tano ya kikazi Mkoani Songwe kuanzia Julai 21 mpaka 25, 2018.

Akitoa taarifa kwa umma kupitia vyombo vya habari ofisini kwake, Mkuu wa Mkoa wa Songwe Chiku Gallawa amemshukuru makamu wa Rais kwa kuupa heshima ya kuutembelea mkoa mchanga ukiwa na miaka miwili tangu uanzishwe.

Gallawa amewataka wananchi wa Mkoa wa Songwe kuipokea heshima hiyo kwa kujitokeza kwa wingi kumlaki makamu wa Rais na kuuonyesha ukarimu wao wa kupenda wageni.

“Wananchi wa Songwe tuna jadi yetu ya kupenda wageni, ni matumaini yangu mtajitokeza kwa wingi hususani maeneo yote ambayo Mgeni wetu atatembelea, mtaonyesha utulivu na amani kipindi chote ambacho atakuwa mkoni kwetu kwakuwa hiyo ndiyo desturi ya wana Songwe”, ameongeza Gallawa.

Ameongeza kuwa tarehe 21 Julai, 2018 Mhe Samia Suluhu Hassan atapokea taarifa ya mkoa na kuzungumza na viongozi na watumishi wa mkoa wa Songwe, tarehe 22 Julai, 2018 atakagua na kukifungua kituo cha Afya cha Nanyala pia atakagua na kuweka jiwe la msingi mradi wa maji Katika kijiji cha Iyula Wilayani Mbozi.

Gallawa amesema tarehe 23 Julai, 2018 Mhe Samia Suluhu Hassan atakuwa Wilaya ya Momba katika halmashauri ya Tunduma ambapo atazungumza na watumishi wote, atakagua na kuzindua Kituo cha Afya cha Tunduma na pia atakagua shughuli za wajasiriamali wa Tunduma.

“Akiwa Wilayani Ileje tarehe 24 Julai, 2018, Mhe Samia Suluhu Hassan atazungumza na watumishi wote, atapokea taarifa ya shughuli za uhifadhi wa mazingira na upandaji wa miti pamoja na kukagua shughuli za uhifadhi na shamba la miti la TFS Katengele”, ameongeza Gallawa.

Gallawa ameeleza kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan atahitimisha ziara yake ya siku tano mkoani songwe tarehe 25 Julai, 2018 kwa kufanya kikao cha majumuisho Wilayani Mbozi na viongozi wote wa mkoa wa Songwe.



Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.