• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MAKOSA YASIRUDIWE UJENZI WA HOSPITALI YA ILEJE- RC MWANGELA

Posted on: April 30th, 2019

  Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brig. Jen. (Mst) Nicodemus Mwangela ameutaka uongozi na watendaji wa Wilaya ya Ileje kusimamia ubora katika ujenzi wa Hospitali ya Ileje ili makosa yaliyojitokeza awali katika ujenzi wa hospitali hiyo, yasijirudie.

Brig. Jen. (Mst) Mwangela ameyasema hapo mapema jana mara baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa Hospitali hiyo ambapo serikali ilitoa shilingi bilioni 1.5 mwezi Disemba 2018 huku majengo yaliyo anza kujengwa yakionekana kuwa na hitilafu za baadhi ya nguzo kupinda na kuwa na nyufa.

“Mkuu wa Wilaya, Mwenyekiti wa Halmashauri, Madiwani na watendaji wote, jengo lilioanza kujengwa na kuwa na nyufa na kupinda pinda liwe funzo kwetu tuhakikishe makosa hayo yasirudie tena katika ujenzi unao endelea sasa, pia wataalamu wote msimamie taaluma zenu na hatutawavumilia endapo mtafanya tofauti” amesisitiza Brig. Jen. (Mst) Mwangela.

Ameongeza kuwa Wananchi wameitikia wito wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli wa kujitolea kwa ajili ya kujiletea maendeleo hivyo basi watendaji wasiwaangushe.

“Serikali imeleta fedha na wananchi wametoa nguvu zao, halafu sisi wataalamu tuiharibu kazi, mimi siko tayari kuona kazi inaharibika, kila mtalaamu atimize wajibu wake, wataalamu wa hospitali wasimamie ujenzi uendane na mahitaji ya hospitali lakini wahandisi wasimamie ubora wa majengo hayo”, ameelekeza Brig. Jen. (Mst) Mwangela.

Brig. Jen. (Mst) Mwangela amesema licha ya ujenzi wa Hospitali hiyo kuchelwa kuanza kwakuwa serikali ilitoa fedha mwezi Disemba 2018, ujenzi huo ufanyike kwa haraka na kwa viwango ili uwe na ubora unaotakiwa na sio kufanya haraka bila kuzingatia ubora huku akiahidi kufanya ukaguzi wa mara kwa mara

 

Amewataka viongozi wa hospitali waliopewa fedha za ujenzi wa hospitali hiyo wawe waaminifu huku akiwataka madiwani kusimamia na kuhoji kwa kufuata taratibu ili waweze kufahamu kila senti ya fedha hizo imetumikaje pia viongozi hao watoe taarifa kwa madiwani kwani ndio wawakilishi wa wananchi ili kuepusha malalamiko kutokana na wananchi kutokuwa na taarifa sahihi.

Aidha Brig. Jen. (Mst) Mwangela amesema kuwa imefikia kipindi cha mavuno hivyo basi madiwani na watendaji wa halmashauri washirikiane katika kukusanya mapato kwani hali ya ukusanyaji mapato sio nzuri

Amewashauri wananchi wachukue tahadhari ya kutouza sana mazao yao kwakuwa si mikoa yote imevuna vizuri hiyvo bei ya mazao inaweza kuwa nzuri zaidi hapo mbeleni hivyo wasifanye haraka kuuza chakula chao na kusisitza kuwa hilo sio katazo kwa wananchi ushauri wa kuchukua tahadhari.

Brig. Jen. (Mst) Mwangela  amewataka Madiwani wasikae na kero na malalamiko ya wananchi bali wawafikishie Wakuu wa Wilaya na Mkuu wa Mkoa ili kero hivo ziweze kutafutiwa ufumbuzi na pia wawahimize wananchi kujitokeza na kueleza kero, maoni na malalamiko yao.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.