• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MAKUNDI NA KUTEGEANA KUMECHELEWESHA MIRADI KUKAMILIKA MOMBA

Posted on: September 26th, 2019

  Uwepo wa makundi yasiyo na tija, kutegeana katika kazi na kutoshirikiana baina ya watumishi kumesababisha miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika halmashauri ya Wilaya ya Momba kuchelewa kukamilika.

Hayo yamebainishwa jana na baadhi ya watumishi wa Halmashauri hiyo walipokuwa wakizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brig. Jen. Nicodemus Mwangela alipokutana nao kutaka kufahamu sababu za kutokamilika kwa wakati ujenzi wa miradi mbalimbali katika halmashauri hiyo.

Mmoja wa watumishi amesema, “unapokuwa na mradi wa sekta fulani mfano afya, kilimo au elimu watumishi wenzako wanakaa pembeni hawakusaidii, ni kama wanakutegea waone utakavyoshindwa kitu ambacho sio sahihi, miradi yote ni ya halmashauri na inalenga kuwanufaisha wananchi wote.”

Watumishi hao wamesema baada ya kuzungumza na Mkuu wa Mkoa wameona kuwa makundi na kutoshirikiana havitaijenga halmashauri na hivyo wameapa kubadilika na kufanya kazi kwa pamoja kama timu moja.

Aidha Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brig. Jen. Nicodemus Mwangela amesema anaamini tatizo la kutoshirikiana baina ya watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Momba limeisha na watafanya kazi kwa pamoja.

Brig. Jen. Mwangela ameongeza kuwa mara baada ya kikao hicho ameona ushirikiano wa watumishi katika ujenzi wa Soko la Mazao la Kakozi ambapo wote kwa pamoja wameonyesha nia kufanikisha ujenzi huo kwakuwa umesha chelewa kwa zaidi ya miezi sita.

Naye Msimamizi wa Ujenzi wa soko la mazao la Kakozi Aloyce Sakaya amesema kwa sasa mradi huo utatekelezwa kwa kasi zaidi kwakuwa changamoto zilizo sababisha ukachelewa ikiwa ni pamoja na kutoshirikiana baina yao zimeondolewa.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.