• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MAMA SAMIA AZINDUA SHAMBA LA MITI LA IYONDO MSIMWA

Posted on: July 24th, 2018

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan amezindua shamba la miti la Iyondo Msimwa lililoko katika kijiji cha Katengele wilayani Ileje lenye hekta zaidi ya elfu 12 na miche zaidi ya laki nne.

Mhe Samia Suluhu Hassan amefanya uzinduzi huo mapema leo ambapo shamba hilo linatarajiwa kutunza vyanzo vya maji 32, kuwaifadhi mbega ambao wako hatarini kutoweka kutokana na kuwindwa hususani na wenyeji pamoja na kutoa ajira kwa wananchi 400.

Amesema shamba hilo linatarajiwa pia kutoa miche elfu 50 kwa wananchi ili wapande hivyo basi wananchi wachangamkie miche hiyo na kupanda kwenye maeneo yao ili kutunza mazingira yaendelee kubaki mazuri na ya kuvutia kama yalivyo.

“Wananchi wa Ileje mmebarikiwa kuwa na mazingira mazuri, wazazi wenu wasingetunza mazingira haya ninyi msingefaidi hali hii nzuri ya hewa nzuri, maji yanatirirka mnalima vizuri, ndugu zangu wa Ileje hasa wa huku Sange na vijiji vya jirani mmepata Baraka kubwa kutoka kwa mungu muitunze”, ameongeza.

Mhe Samia Suluhu Hassan amesema kuwa amesikitishwa na wananchi kujenga katika milima na kukata miti yote katika maeneo ya milimani hali ambayo itasababisha kukosekana mvua, mito kukosa maji hali itakayopelekea kukosekana kwa maji.

“Tusipotunza mazingira yatatuadhibu, vyanzo vya maji vikiharibiwa pia tutapata magonjwa na maji tutakosa na hiyo ndiyo adhabu yenyewe…, lakini pia tunazo sheria na miongozo inayoongoza utunzaji mazingira ambazo zina adhabu zake kwa yeyote anayeharibu mazingira ata adhibiwa”, amesisitiza.

Naye Murugenzi wa Rasilimali misitu kutoka Wakala wa Huduma za Misitu (TFS) Mohamed Kilonzo amesema baadhi ya changamoto za shamba hilo la miti ni pamoja na wananchi kuvamia baadhi ya maeneo ya samba hilo na mifugo kuingia ndani ya shamba hali inaopelekea uharibifu wa miti inayopandwa.

Kilonzo amesema ili kukabiliana na changamoto hiyo TFS imetoa elimu kwa wananchi juu ya madhara ya mifugo kuingia ndani ya hifadhi na wananchi wameanza kuelewa umuhimu wa shamba hilo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.