• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MAMIA WAFURIKA KUPIMA VVU SONGWE

Posted on: October 2nd, 2018

  Mamia ya wananchi Mkoani Songwe wamejitokeza kupima maambukizi ya Virusi Vya Ukimwi (VVU) katika shule ya Sekondari Nalyelye Mlowo wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Upimaji VVU na kuanzishiwa dawa za kupunguza makali (ARV) ijulikanayo kama Furaha yangu Pima, Jitambue, Ishi.

Uzinduzi wa Kampeni hiyo ya Furaha yangu umefanywa na Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brigedia Jenerali Nicodemus E Mwangela mwishoni mwa wiki ambapo katika siku hiyo wananchi 367 wamejitokeza kupima VVU, kati yao wanaume 208 na wanawake 159 huku kampeni hiyo ikisisitiza zaidi wanaume kupima VVU kutokana na takwimu kuonyesha wanaume wachache ndio hupima.

“Wanaume tumekuwa na tabia ya kuwatanguliza wake zetu kupima VVU, sasa tufanye tofauti, sisi wanaume ndio tuongoze wafuate akina mama, tukipima tukajua afya zetu tutaweza kuishi kwa furaha, hata ukibainika kuwa na maambuzi ya VVU utaanzishiwa dawa mara moja hii itasaidia kuimarisha afya yako na utaendelea kuishi kwa furaha”, amesisitiza Brig. Jen. Mwangela.

Ameongeza kuwa wananchi wajenge tabia ya kupima afya zao hata katika magonjwa mengine kama ambavyo imefanyika katika uzinduzi wa kampeni hiyo ambapo wananchi 320 walijitokeza kupima kisukari na shinikizo la damu, wanaume 30 walijitokeza kufanyiwa tohara na katika kuchangia damu zilipatikana chupa 34.

Kwa upande wake Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Songwe Dkt. Kheri Kagya amesema kampeni ya Furaha yangu imetoa picha ya kuwa wananchi wengi bado wana uhitaji wa kupima VVU na magonjwa mengine yasiyo ambukiza ili wapate huduma mapema kabla hawajapata madhara makubwa, hivyo basi kila halmashauri zitaweka utaratibu wa upimaji afya angalau mara moja kwa mwezi kwa kuwafuata wananchi katika ngazi za vijiji na kata.

Dkt Kagya amesema hamasa kubwa ilifanyika kwa njia mbalimbali na wananchi walihamasika kufika kwenye uzinduzi kwa wingi na pia kujitokeza kupima kwa wingi, matumaini ya Mkoa ni kuwa wananchi wameelewa kuwa furaha yangu ni kupima VVU kutambua hali zao za kiafya ili waishi kwa amani na furaha

Mkazi wa Mlowo Wilfred Myatege aliyejitokeza kupima amesema kupima afya ni muhimu kwa kila mmoja kwa kuwa mtu anaweza kuwa na magonjwa na asijitambue mapema mpaka madhara makubwa yatakapojitokeza.

Myatege ameongeza kuwa wananchi wengine hudhani kuwa wamerogwa baada ya kupata madhara ya magonjwa ambayo wangeyatambua mapema wasingedhurika sana, hivyo basi fursa hiyo ya upimaji waitumie vizuri kutambua hali zao mapema.

Katika kipindi cha mwaka 2016 watu 71,000 walijitokeza kupima VVU Mkoani Songwe ambapo wanaume walikuwa asilimia 41.4 na katika kipindi cha mwaka 2017 waliopima VVU ni 129,853 wanaume walikuwa asilimia 45.6 ambapo asilimia ya maambukizi ilikuwa 5.8.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC CHONGOLO AONGOZA KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI WILAYA YA MOMBA KUJADILI HOJA ZA CAG

    June 11, 2025
  • RC CHONGOLO AONGOZA KIKAO CHA KUJADILI HOJA ZILIZO BAINISHWA KATIKA RIPOTI YA CAG HALMASHAURI YA MBOZI

    June 10, 2025
  • RC CHONGOLO APIONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA ILEJE KWA KUPATA HATI SAFI

    June 10, 2025
  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.