• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MAZOEZI HUPUNGUZA MAGONJWA YASIYO AMBUKIZA

Posted on: September 11th, 2019

 Mganga Mkuu wa Mkoa wa Songwe Dkt Kheri Kagya ametoa rai kwa wananchi wote Mkoani Songwe kuwa na tabia ya kufanya mazoezi ya viungo mara kwa mara ili kuufanya mwili ubaki na uzito unaotakiwa na hivyo kupunguza magonjwa yasiyo ambukiza.

Dkt Kagya amesema hayo wakati wa mazoezi ya Viungo yaliyoongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brig. Jen. Nicodemus Mwangela katika Wilaya ya Ileje lengo likiwa kuhamasisha wananchi kujenga mazoea ya kufanya mazoezi mara kwa mara.

Amesema kwa sasa kumekuwa na ongezeko kwa asilimia 33 la vifo vitokanavyo na magonjwa yasiyoambukiza kama vile shinikizo la damu na kisukari ambavyo hupatikana hasa kwa kutofanya mazoezi mara kwa mara.

“Mazoezi ni nyenzo muhimu ya kuzuia magonjwa yasiyoambukiza na inashauriwa angalau kwa siku mtu ufanye mazoezi kwa dakika 30 na waliojitokeza kufanya mazoezi leo wasiache kwani watapata maumivu makali na pia hawataweza kuiona faida ya mazoezi katika afya zao”, amesema Dkt Kagya.

Dkt Kagya ameongeza kuwa miaka ya 1990 vifo vitokanavyo na magonjwa yasiyo ambukiza vilikuwa asilimia 19 lakini sasa vifo hivyo vimefikia asilimia 33 na hii imesababishwa na watu kuacha misingi ya kufanya mazoezi ya mara kwa mara.

“Ongezeko la vifo vitokanavyo na magonjwa yasiyo ambukiza linasababishwa na kuacha misingi ya mazoezi, vitambi sio dili tena, tufanye mazoezi ili kupunguza uzito usiohitajika kwani kwa sasa tunao watu wengi wenye uzito ulio zidi wastani na uliopitiliza”, amesisitiza Dkt Kagya

Ameongea kuwa mazoezi ni muhimu ili kujenga afya bora ya mwili na akili na hasa akina mama wengi ambao wamekuwa wakihisi kuwa mazoezi ni kwa ajili ya wanaume tu, hivyo basi wasisubiri matukio bali wafanye mazoezi mara kwa mara kwani afya bora ni mtaji wa kufikia uchumi wa kati.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brig. Jen. Nicodemus Mwangela amewashukuru wananchi wa Mkoa wa Songwe hususani wa Wilaya Ileje waliojitokeza kwa wingi kufanya mazioezi ili kujenga afya zao.

Brig. Jen. Mwangela amesema mazoezi hujenga afya bora na uhusiano mzuri hivyo anawapongeza wote walioshiriki hususani wanawake na watoto walioshiriki kuanzia mwanzo wa mbio (jogging) mpaka mwisho wapewe hamasa ya kuendelea na mazoezi.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Ileje Jonas Mkude amemshukuru Mkuu wa Mkoa wa Songwe kwa kuhamasisha wananchi Kufanya mazoezi ili kuboresha afya zao.

Mkude amesema wananchi wa Ileje wanapenda mazoezi na Michezo hivyo wataendelea kufanya mazoezi mara kwa mara ili kujenga afya na kukuza michezo Wilayani humo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.