• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MKUU WA MKOA WA SONGWE AAGIZA KUREJESHWA SHULE MWANAFUNZI ALIYEKATISHA MASOMO NA KWENDA KUWA 'HOUSE GIRL'.

Posted on: November 14th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Dkt Francis  Michael, amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Ileje, Frida Mgomi kuhakikisha anamrejeaha shuleni mwanafunzi wa kidato cha kwanza katika shule ya wasichana (Ileje Girls) anayedaiwa kukatisha masomo na kwenda kufanya kazi za ndani ili aendelee na masomo.

Pamoja na hilo, Dkt. Michael

pia ameagiza

Kurejeshwa shuleni hapo kwa wanafunzi wengine watatu ambao wazazi wao

waliwahamisha na kuwapeleka katika shule za kutwa kwa kisingizio cha wazazi kukosa michango ya chakula.


Mkuu wa mkoa Dkt. Michael, Ametoa maagizo hayo November 14, 2023,  wakati akitimiza ahadi yake ya kuwapatia kila mwanafunzi daftari tano (Counter book)  wanafunzi wote wa shule hiyo.


Awali akitoa taarifa ya shule, Kaimu Mkuu wa  shule hiyo, Sharon Kadinde, alisema shule hiyo ya wasichana iliyoanzishwa mwaka huu ilipangiwa wanafunzi 75 , lakini walioripoti shuleni hapo ni 71 tuu.


Aliongeza kuwa  mwanafunzi mmoja alikatiza masomo kwa shinikizo la wazazi wake, huku wanafunzi wengine watatu akidai kuwa, licha ya kuripoti shuleni hapo wazazi wao waliwahamisha na kuwapeleka katika shule za kutwa kwa madai ya kutokuwa na uwezo wa kuchangia chakula.


" Baada ya wazazi wake kumshinikiza aacha shule, tulifuatilia na kubaini kuwa  mwanafunzi huyo kwa sasa anafanya kazi ndani  katika mji wa Tunduma . Alieleza Kaimu Mkuu wa shule hiyo.


Kufuatia taarifa hiyo, Mkuu wa Mkoa alimtaka mkuu wa wilaya hiyo, kuwafuatilia wazazi wa mwanafunzi huyo ili wamrudishe mwanafunzi huyo aendelee na masomo.


" Mwanafunzi huyu atakapo rudi shule Mkurugenzi hakikisha unampatia mchango huo wa chakula ili aweze kutimiza ndoto zake za kupata elimu.. tena nimeambiwa mwanafunzi huyo ana uwezo mkubwa darasani" alisisitiza Mkuu wa Mkoa.


Katika hatua nyingine, Dkt. Michael imewaonya wazazi wenye tabia za kuwakatisha masomo Wanafunzi amewataka kuacha mara moja kwa sababu watakaobainika watakamatwa na kuchukuliwa Hatua kali za kisheria.


Baadaya ya maelekezo hayo, Mkuu wa Mkoa alikagua Maendeleo ya Ujenzi wa majengo mawili ambayo ni nyumba moja ya Mwalimu itakayotumiwa na familia mbili, inayogharimu kiasi cha sh. Milioni 100 ambazo ni fedha kutoka serikali Kuu.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.