• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MPANGO WA UONGEZAJI VIRUTUBISHI WAZINDULIWA MKOANI SONGWE

Posted on: May 31st, 2018

  Mpango wa uongezaji virutubishi katika unga wa mahindi umezinduliwa rasmi Mkoani Songwe huku Mkuu wa Songwe Chiku Gallawa akiwataka wataalamu na taasisi zinazohusika na lishe kusimamia suala la ubora wa chakula kwakuwa linagusa maisha ya binadamu.

Gallawa amesema mpango huo utasaidia kupunguza kiwango cha udumavu ambacho kwa sasa ni asilimia 37.7 hali ambayo haikubaliki kutokana na uwepo wa vyakula vya kutosha mkoani hapa.

“Mkoa wa Songwe kubaki na asilimia kubwa ya udumavu, utapiamlo na ukondefu haikubaliki, vyakula vipo, kilichobaki ni wataalamu wa lishe kufanya kazi yenu ya kuelimisha namna ya kuchanganya vyakula hivyo vilete afya bora na mafunzo hayo yafike mpaka ngazi ya vijiji”, amesisitiza Gallawa.

Ameongeza kuwa masuala ya chakula yanagusa usalama wa wananchi hivyo Mkoa wa Songwe umejipanga kufikia malengo ya maendeleo hasa kwa kutumia taarifa, takwimu sahihi na mipango inayotekelezeka.

“Hatutaki maneno ya ubabaishaji, tunahitaji takwimu na taarifa sahihi, tumejipanga kuelekea kwenye uchumi wa viwanda utakaojengwa na wananchi wenyewe wakiwa na afya bora hivyo basi taasisi zote zinazohusika na masuala ya chakula mkija Songwe muwe na mikakati inayotekelezeka”, amefafanua.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mradi wa NAFAKA nchini Silas Ng’habi amesema malengo ya mradi wa uongezaji virutubishi unoafadhiliwa na shirika la kimataifa la USAID ni kuwapa wananchi chakula kilicho bora.

Amesema viinilishe vitakavyowekwa katika unga wa mahindi vitajenga jamii yenye afya bora na hivyo kupata wabunifu wa teknolojia mbalimbali pamoja na kuwajenga watoto wenye ufahamu mkubwa.

Naye Afisa Lishe kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Elizabeth Ndaba amesema kuwa virutubishi vitakavyoongezwa katika unga wa mahindi ni salama kwakuwa vimekaguliwa na kuhakikiwa na shirika la viwango nchini (TBS) ili kuangalia ubora wake pamoja na Mamlaka ya Chakula na Dawa Nchini (TFDA) Kuangalia usalama kwa watumiaji.

Ndaba amesema mpango wa uongezaji virutubishi umelenga kupunguza hali ya udumavu nchini ambayo ni asilimia 34 huku akifafanua kuwa udumavu hudhoofisha afya ya mwili na uwezo wa kiakili hali ambayo pia huathiri katika uzalishaji na ukuaji wa uchumi nchini.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.