• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MSISUBIRI SERIKALI ISEME, PANDENI MITI-RC MWANGELA

Posted on: April 1st, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brig. Jen. Nicodemus Mwangela ametoa rai kwa wananchi wote kujenga mazoea ya kupanda miti bila kusubiri maagizo au maelekezo kutoka serikalini ya kuwataka kufanya hivyo.

Brig. Jen. Mwangela ametoa rai hiyo mapema leo katika chanzo cha maji cha Ilolo Wilayani Mbozi wakati wa maadhimisho ya siku ya kitaifa ya Upandaji Miti ambapo kwa Mkoa wa Songwe maadhimisho hayo yamefanyika kwa viongozi mbalimbali kupanda miti.

Amesema wananchi wajenge tabia ya kupanda miti kwa wingi kwakuwa miti ina faida nyingi na pia Mkoa wa Songwe una ardhi nzuri ambayo inawezesha aina nyingi za miti kustawi.

Brig. Jen. Mwangela ameongeza kuwa licha ya Mkoa wa Songwe kuwa na hali ya hewa nzuri, kipaumbele kiwe ni kupanda miti kwa wingi kwakuwa isipo fanyika hivyo itafikia kipindi mvua zinazo patikana hivi sasa hazitakuwepo.

Aidha ameziagiza halmashauri za Wilaya kuhakikisha zinatunza vizuri vyanzo vya maji na mikakati inawekwa ya kuhakikisha miti inayopandwa yote inakua vizuri ikiwa ni pamoja na kutorusu mifugo kusambaa na kuharibu vyanzo vya maji.

Afisa Maliasili Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi Charles Ndimbo amesema kwa sasa wanaendelea kuwahamasisha wananchi kujengea wigo katika maeneno yote waliyopanda miti na kuzuia mifugo yao isizurure na kufanya uharibifu.

Ndimbo amesema Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi inasimamia misitu 70  huku Lengo likiwa ni kupanda miti milioni mbili kwa Mwaka Lakini kwa mwaka 2018/2019 zaidi ya miti milioni 1.6 ilipandwa huku iliyofanikiwa kukua ikiwa ni miti milioni 1.1.

Amesema kuna sababu mbalimbali zinazopelekea miti inayopandwa kushindwa kukua ikiwa ni pamoja na miti hiyo kupandwa katika maeneo yasiyo faa, kuliwa na wadudu, kuharibiwa na mifugo, ukame pamoja na kuchomwa moto.

Nao baadhi ya wananchi walioshiriki maadhimisho ya siku ya upandaji miti wameiomba serikali kuendelea kuwachukulia hatua kali za kisheria wote wanao haribu miti.

Kaulimbiu ya kitaifa ya maadhimisho ya Siku ya Upandaji miti kwa mwaka 2020 ni, “Tutunze Mazingira, tukabiliane na Mabadiliko ya tabia Nchi”.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.