• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MVUA ZAHARIBU NYUMBA ZAIDI YA 360 SONGWE

Posted on: November 20th, 2019

  Mvua iliyoambatana na upepo mkali iliyonyesha jana jioni Mkoani Songwe imesababisha uharibifu wa nyumba Zaidi ya 360 Katika Wilaya za Mbozi na Momba pamoja na kujeruhi watoto wawili.

Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brig. Jen Nicodemus Mwangela mapema leo ametoa taarifa hiyo mara baada ya kukagua hali ya uharibifu wa makazi ya watu na taasisi za serikali ambapo ameziagiza halmashauri husika kurejesha miundombinu ya serikali iliyoharibika.

“Kuna wananchi wamepata madhara lakini wametibiwa na kurejea nyumbani, nawapongeza sana viongozi na majirani ambao waliwahi kutoa msaada kwa wahanga aidha ninaagiza halmashauri za Momba na Mbozi warekebishe haraka nyumba za walimu na madarasa ili huduma ziendelee.”, amesema Brig. Jen. Mwangela.

Aidha ametoa pole kwa wahanga  na amewapongeza majirani wa waliopata uharibifu wa nyumba kwa kuwahifadhi wenzao jana usiku huku akiwa hakikishia kuwa Kamati za Usalama za Wilaya na wataalamu wanafanya tathmini ya uharibifu na kupanga namna ya kutoa msaada.

Brig. Jen. Mwangela amewataka wananchi wote kuchukua tahadhari kwakuwa mvua za Mkoani Songwe ni nyingi hivyo waimarishe makazi yao pia watoe taarifa mapema endapo utatokea uharibifu wowote.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mbozi Hanji Godigodi amesema wataalamu wa Halmashauri wanaendelea na tathmini ya hali ya uharibifu na kuwa nyumba za walimu na shule zitafanyiwa marekebisho haraka.

Afisa Mtendaji kata ya Msangano Halmashauri ya Wilaya ya Momba Focus Kadule amesema baada ya tathmini ya hali ya uharibifu katika kata yake ataitisha Mkutano wa hadhara ili wananchi waweze kujitolea kuwasaidia waliopata uharibifu kutokana na mvua hizo.

Fadeli Ng’aala mkazi wa Kijiji cha Hamwelo Halmashauri ya Mbozi amesema mvua iliyoambatana na upepo imeezua paa la nyumba yake huku yeye na watoto wakiwa ndani na kusababisha uharibifu wa vyakula na vifaa vingine kama vitanda, magodoro, televisheni, solar na masofa.

Naye Mwalimu Jacob Sambilila wa Shule ya Msingi Nkala Halmashauri ya Wilaya ya Momba amesema mvua zilianza saa tisa mchana na kusababisha mti kuangukia darasa hali iliyozua taharuki kwa wanafunzi lakini pia baada ya kurudi nyumbani kwake alikuta nyumba anayoishi imeezuliwa.

“Baada ya kutoka kazini nilikuta nyumba ya mwalimu mwenzangu imeezuliwa na nilipofika kwangu nimekuta nyumba imebomoka na kuezuliwa na kusababisha uharibifu hata kwenye chakula chote nilichotunza kimeharibika na vifaa vya ndani.”, amesema Mwalimu Sambilila.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.