• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

NAIBU WAZIRI KANDEGE AAGIZA KITUO CHA AFYA LUBANDA KIKAMILIKE KWA WAKATI

Posted on: July 19th, 2018

Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) Josephat Kandege jana amefanya ziara ya kikazi Wilaya ya Ileje kukagua ujenzi wa kituo cha Afya cha Lubanda na kuagiza ujenzi wa kituo hicho ukamilike kwa wakati uliopangwa.

Kandege amesema uwepo wa mvua nyingi ambazo huanza mapema katika wilaya hiyo utakwamisha kituo hicho kukamilika mapema endapo hawatautumia muda huu ambao hauna mvua kumalizia ujenzi kwa haraka.

“Ninaamini kama isingekuwa mvua nyingi kunyesha pamoja na kuharibika kwa barabara nimatumaini yangu ujenzi wa kituo hiki cha Afya ungekuwa umekamilika, sasa jitahidini kumaliza haraka kabla ya mvua kuanza, ili mradi huu ukamilike na uanze kuwanufaisha wananchi wa Lubanda na maeneo ya jirani”, amesisitiza Kandege.

Aidha amemuelekeza Mganga Mkuu wa Wilaya ya Ileje Enock Mwambalaswa kubana matumizi ya fedha zilizotolewa kwa ajili ya ujenzi wa kituo hicho ili fedha zitakazobaki zitumike kumalizia jengo  la wazazi na wagonjwa wa nje ambalo lilianza kujengwa kwa nguvu za wananchi pamoja na kujenga nyumba nyingine za watumishi.

Kandege amemuelekeza pia Mhandisi wa Halmashauri ya Ileje kuangalia uwezekano wa kuunganisha wodi ya wazazi na chumba cha upasuaji ili kuendana na ramani mpya za vituo vya afya, aidha ameelekeza utaratibu wa kufikisha umeme kituoni hapo hasa kupita mpango wa REA uanze kufanyika haraka.

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ileje Haji Mnasi amemueleza Naibu Waziri OR TAMISEMI Josephat Kandege kuwa halmashauri ilipokea shilingi milioni mia tano kwa ajili ya ujenzi wa kituo hicho cha Afya cha Lubanda na mpaka sasa ujenzi umefikia asilimia 95 na matarajio ni kuwa kituo hicho kitakamilika ifikapo Julai 25, 2018.

Mnasi amemshukuru Naibu Waziri Kandege kwa kufanya ziara ya kukagua kituo hicho na amemuhakikishia kuwa atazingatia maelekezo ya kuwapangia watumishi wapya wa sekta ya afya watakaoajiriwa hivi sasa katika vituo vya afya vinavyojengwa ili vitoe huduma kwa wananchi mara baada ya kukamilika.



Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.