• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WANAWAKE WAHIMIZWA KUCHANGAMKIA FURSA YA KUCHIMBA MADINI

Posted on: April 6th, 2018

  Mkuu wa Mkoa wa Songwe Chiku Gallawa amewahakikishia wanawake wa kijiji cha Saza Wilaya ya Songwe kuwa wanaweza kufanya kazi ya kuchimba madini hivyo wachangamkie fursa hiyo.

Gallawa ameyasema hayo mapema leo alipowatembelea wanawake waliokuwa wakipewa elimu ya uchimbaji madini katika kijiji cha Saza ambapo baadhi yao walionekana kuwa na mashaka endapo mwanamke anaweza kuingia ndani ya mgodi na kuchimba madini.

“Nimeshuhudia kwa macho yangu wanawake wanachimba madini tena kwa kutumia sululu, ninyi mtashindwa kweli?!, wanawake wana nguvu na akili nyingi, msijishushe hakuna kazi ya mwanaume na mwanaume, sasa hivi kuna wahandisi wanawake kila idara, marubani na viongozi wakubwa tu”, amesisitiza Gallawa.

Ameongeza kuwa mara baada ya mafunzo hayo ya Afya na Mazingira, usalama migodini na sheria za madini wanawake hao wanapaswa kujiunga katika vikundi ili serikali iweze kuwafikia kwa urahisi.

“Najua wanawake wengi tuna historia ya kufanya vizuri kwenye vikundi naimani baada ya mafunzo haya mtajiunga kwenye vikundi na ninamuagiza afisa maendeleo ya jamii arudi tena kutoa mafunzo ya ushirika ili muelewe vizuri”, amefafanua Gallawa.

Gallawa amesema vikundi hivyo vitasaidiwa kuandaa andiko la mradi, kuwapa mafunzo Zaidi, kupatiwa leseni na mitaji yao ambayo itakuwa mikopo kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Wizara ya Madini na mifuko mbalimbali.

Naye Mkazi wa Kijiji cha Saza Wilaya ya Songwe Bi Elimina Atanasi ameiomba serikali licha ya kutoa mafunzo hayo ya uchimbaji, itenge maeneo ya uchimbaji kwa ajili ya wachimbaji wadogo hasa vikundi vya akina mama.

Bi Atanasi amesema wachimbaji hao wadogo hasa wanawake wamekuwa wakipata shida ya kuondolewa katika maeneo wanayochimba jambo ambalo linawafanya wakose fedha za kukidhi mahitaji yao.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.