• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RAIS SAMIA ARIDHIA WANANCHI WA NKANKA KUBAKI KWENYE HIFADHI.

Posted on: October 24th, 2022

RAIS SAMIA ARIDHIA WANANCHI WA NKANKA KUBAKI KWENYE HIFADHI.

ILEJE: Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan ameridhia wananchi wapatao 3,000 wanaoishi katika hifadhi ya msitu wa Ileje Renger iliyopo kitongoji cha Nkanka Kijiji cha Itumba wilayani Ileje kuendelea kubaki kwa kuhakikisha wanatunza Mazingira wakati Serikali inaandaa utaratibu wa kuweka mipaka rasmi ya kitongoji hicho.

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa kamati ya mawaziri wa kisekta inayoshughulikia migogoro ya Ardhi, Mhe. Dkt. Angelina Mabula ambaye ni Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi wakati wakiongea na wananchi wa kitongoji cha Nkanka Oktoba 24.

Dkt. Angelina Mabula ametoa miezi 2 kwa watalamu kuhakikisha wanatambua mipaka halisi ya kitongoji cha Nkanka ili wananchi wajue ni wapi wanaishia.

"Baada ya mipaka kuwekwa hatutarajii kuona mwananchi anaingia kwenye eneo la hifadhi, ukifanya hivyo ni kukiuka makubaliano na utachukuliwa hatua za kisheria" Dkt. Angelina Mabula.

Pia, Waziri wa Ardhi, Mhe. Dkt. Angelina Mabula ametoa wito kwa wananchi wa kitongoji cha Nkanka kuepuka kugawa Ardhi hovyo kwa wageni bila utaratibu, kwani Serikali haijafungukia milango kwa wageni kuvamia eneo ili ila wataingia kwa kufuata utaratibu.

Mhe. Dkt. Mabula amewataka watalamu kwa kushirikiana na wananchi wanapokwenda kupanga mpango bora wa matumizi ya Ardhi waweze kuzingatia sehemu ya huduma za jamii, Kilimo, mifugo pamoja na akiba kwa maendeleo ya Nkanka kwa miaka ijayo kutokana na eneo lao haliwezi kuongezwa.

Agnes Nyondo mwananchi wa kitongoji cha Nkanka amesema baada baadhi ya viongozi kuwaambia wahame wamejikuta wanashindwa kufanya mambo ya maendeleo, kama kujenga kulima kwani wamekuwa wakiishi kwa hofu, lakini tunamshukuru sana Rais wetu Mama Samia kwa uhamuzi wake wa sisi kuendelea kubaki hapa.

Ephraim Kayinga mkazi wa kitongoji cha Nkanka amewaomba mawaziri kuwafikishia salama kwa Rais Samia kwa uamuzi wake wa kuwabakiza kwani wao wamezaliwa Nkanka na maisha yao yoote yamekuwa hapa.

MWISHO

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI DATA CLEARK, CLINICIAN NA NURSE October 01, 2021
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANAWAKE WAGUSA MAISHA YA WATU WENYE WAHITAJI

    March 08, 2023
  • WITO WATOLEWA WANAWAKE KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI ZILIZOPO.

    March 06, 2023
  • NIMEKUJA KUBORESHA MAZURI YOTE, RC MICHAEL.

    March 03, 2023
  • TUTAFANYA KAZI NA WADAU WOTE KUTIMIZA LENGO LA SERIKALI: RC MICHAEL.

    March 02, 2023
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras.songwe@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.