• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RAS SENEDA ATAKA MIGOGORO YA ARDHI ITATULIWE NA HALMASHAURI KABLA HAIJAFIKA MKOANI.

Posted on: September 23rd, 2022

RAS SENEDA ATAKA MIGOGORO YA ARDHI ITATULIWE NA HALMASHAURI KABLA HAIJAFIKA MKOANI.

SONGWE: Katibu Tawala Mkoa wa Songwe, Bi. Happiness Seneda amewagiza viongozi wa Halmashauri kwa kushirikiana na watalamu wa Ardhi kutatua migogoro yote ambayo ipo kwenye maeneo yao kabla haijafika ngazi ya Mkoa.

Katibu Tawala wa Mkoa ametoa maagizo hayo wakati wa kikao kazi cha sekta ya Ardhi kilichowakutanisha watalamu wote wa Ardhi pamoja na wakurugenzi wa Halmashauri zote za Mkoa kilichofanyika Septemba 23 Mkoani Nselewa.

Bi. Happiness Seneda amesema migogoro yote ya Ardhi inatakiwa kutatuliwa na Halmashauri kwani Mkoa hauna Ardhi isipokuwa tu kwa migogoro ambayo Mkoa unaweza kushauri au kufanya jambo ili kumaliza mgogoro wa huo.

Katika kufanikisha utatuzi wa migogoro ya Ardhi lazima tufanye kazi kama timu moja kwa ushirikiano mkubwa hakuna mtu wa kujiona yeye ndio yeye.

Serikali itafuatilia kwa karibu sana kuona kama mnafanya kazi kama timu na kwa kushirikiana, kwani eneo la Ardhi ndio kipaumbele chetu amesema, Bi. Happiness Seneda.

Pia, Bi. Happiness Seneda amesema anataka kuona eneo la Mkoa linapimwa na kupangika vizuri kwa kutumia fedha za Serikali au kwa kushirikiana na sekta binafsi.

Watalamu wa Ardhi kutoa ushirikiano mzuri kwa mtu mwenye eneo lake ambaye anahitaji lipimwe ili tuweze kuongeza maeneo mengi yaliyopimwa na tusiwatie hofu juu ya gharama kubwa za upimaji ila tuwape mbinu bora na nzuri za kufanikisha, amesema, Bi. Happiness Seneda.

Aidha, Katibu Tawala Mkoa wa Songwe, Bi. Happiness Seneda ameziagiza Halmashauri zilizopata fedha za upimaji viwanja kuanza kurejesha fedha izo ili zikafanye kazi nyingine za Serikali.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Tunduma, Ndg. Philemon Magesa ametoa wito kwa watalamu wa Ardhi kushirikiana kwa Karibu na ofisi za wakurugenzi ili waweze kutatua changamoto kwa pamoja, na wasiwe watu wa kujitenga kujiona wao sio sehemu ya Halmashauri.

Ndg. Magesa amesema swala la kupima Ardhi, watalamu wa Ardhi wakiamua na kujituma kwa ushirikiano na Mkurugenzi wanaweza kupima Ardhi eneo kubwa sana kwa kutumia Rasilimali zilizopo.

"Mfano Tunduma tumeweza kutumia fedha za mapato ya ndani zaidi ya milioni 15 na tumefanikiwa kupima viwanja zaidi ya 600 hivyo jambo ili linawezekana swala watalamu wa Ardhi wasiwe mbali na Halmashauri" Philemon Magesa.

Aidha, Ndg. Magesa amesema watalamu wa Ardhi wakijipanga vizuri wanaweza kutatua migogoro yote na ikaisha, kama sisi Tunduma tulianza kuunda timu ya kuitambua na migogoro yote ya Ardhi na kuisajili, tumeitambua na tumeanza kuchukua hatua za kutatua kwa wananchi kuwapatia viwanja kwenye mpango huu ambao tumeanza kupima.

Kaimu Kamishina wa Ardhi Mkoa wa Songwe, Winfrida Mwasulama amewataka watalamu wenzake kufanya kazi kwa ushirikiano ili kufanikisha kwani kazi za Ardhi mtu moja asipotekeleza jukumu lake vizuri basi mwingine naye hawezi kufanya kwa ufasaha.

Kwa upande wake, Kamishina wa Ardhi Mkoa wa Mbeya, Syabumi Mwaipopo amewataka wakuu wa Idara za Ardhi kuwatumia vizuri vijana wanaojitolea ili kuweza kutekeleza majukumu vyema ya Mipango ya Ardhi.

Wakati huo huo, Katibu Tawala Mkoa wa Songwe, Bi. Happiness Seneda amesisitiza ukusanyaji wa Kodi ya Ardhi na kuwataka watalamu wa Ardhi kuwakunbusha wananchi juu ya msamaha uliotolewa na Serikali kwa wanaodaiwa Kodi ya Ardhi.

MWISHO.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.