• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC ASHAURI VIWANDA VYA ALZETI KUFANYIWA MABORESHO YA KUCHAKATA MAZAO MENGINE YA MAFUTA.

Posted on: July 14th, 2022

RC ASHAURI VIWANDA VYA ALZETI KUFANYIWA MABORESHO YA KUCHAKATA MAZAO MENGINE YA MAFUTA.

SONGWE: Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Omary Mgumba ametoa ushauri kwa wamiliki wote wa viwanda vya kusindika alzeti nchini kuweza kuvifanyia maboresho viwanda vyao ili viweze kusindika mafuta kwa kutumia mazao mengine jamii ya mafuta kama vile soya, karanga na michikichi.

Mkuu wa Mkoa wa ametoa ushauri huo alipofanya ziara katika kiwanda cha kusindika mafuta ya alzeti cha Majinja kilichopo wilayani Mbozi Julai 14 na kukuta moja ya changamoto ya kiwanda ni ukosefu wa malighafi kulingana na uwezo wa kiwanda.

Mkuu wa Mkoa amesema changamoto ya upatikanaji wa malighafi ni tatizo la nchi nzima kwani viwanda vilivyopo sasa vinauwezo wa kuzalisha tani milioni 2 kwa mwaka lakini mahitaji ya nchi ni tani milioni 1.5 lakini viwanda vilivyopo sasa vinazalisha zaidi ya tani laki 5 kwa mwaka na kufanya nchi kuagiza mafuta kutoka nje kwani uzalishaji uko chini.

“Kwa sasa viwanda vinahitaji kuzalisha tani milioni 1.4 lakini kutokana na ukosefu wa malighafi ya alzeti vinazalisha na kufanya viwanda vizalishe chini ya tani laki 6 kwa mwaka” Mhe. Omary Mgumba.

Kutokana na changamoto hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Omary Mgumba ametoa wito kwa wamiliki wa viwanda vya kuchakata mafuta ya alzeti kubadili mfumo wa viwanda vyao ili viweze kuchakata mafuta ya soya pale ambapo wanakuwa wamekosa malighafi ya alzeti.

Mfano wananchi walio wengi wa Mkoa wa Songwe wananunua mafuta ya kupikia kutoka nchi ya Zambia ambayo yametengenezwa kwa soya, na sisi hapa tunalima soya kalanga hivyo ni wakati sasa wamiliki wa viwanda hivi kwenda kujifunza Zambia au kokote kule ili viwanda vianze kuchakata mafuta kwa mazao mbadala ya mafuta nasio kutegemea zao la alzeti tu.

Mkurugenzi wa kiwanda cha Majinja, Ndg. Alnanuswe Kabungo  ameiomba Serikali kuhamasisha wakulima waweze kulima alzeti na kuichukua lazeti kama zao lao mbadala baada ya mazao waliyoyazoe ili Serikali iondokane nan a kuagiza mafuta kutoka nje ya nchi kwani kwa sasa ardhi ipo ya kutosha ni swala la wakulima wapewe elimu ili waweze kulima kwa ajili ya viwanda vyetu.

Aidha, Mkurugenzi wa Majinja, Bwn. Kabungo amesema ataufanyia kazi ushauri wa Mkuu wa Mkoa na ameishukuru Serikali ya Mkoa wa Songwe kwa kuweka mazingira rafiki ya kuwekeza ndani ya Songwe kwa kuweze kuimarisha ulinzi na usalama na wao kujisikia raha kusihi Songwe.

Akisoma taarifa ya kiwanda, Bwn. Agrey Kandonga amesema ifikapo Agosti 2022 kiwanda kitaanza uzalishaji wa tani eflu 12 za mafuta kwa mwaka sawa na lita laki 240,000 na mafuta yatakayozalishwa yatakuwa yanasafishwa mara mbili kwa ubora wa kimataifa.

Kiwanda cha kuchakata mafuta ya alzeti cha Majinja hadi kukamilika kwake kitagharimu kiasi cha fedha shilingi milioni 730 na kitakuwa msaada kwa wakulima wa Alzeti waliopo Mkoa wa Songwe.

MWISHO.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.