• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC MAKAME AONGOZA JUKWA LA WADAU WA KILIMO MKOANI SONGWE.

Posted on: November 19th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mheshimiwa Jabir Omari Makame, leo amefungua rasmi Jukwaa la Wadau wa Kilimo la Mkoa wa Songwe, hafla iliyowakutanisha wataalam, viongozi wa taasisi mbalimbali, wakulima, wawekezaji na wadau wengine muhimu wa sekta ya kilimo. Tukio hilo limefanyika kwa lengo la kujadili kwa pamoja nafasi, changamoto na fursa zilizopo katika sekta hiyo ili kuongeza tija na kuinua uchumi wa wananchi wa Songwe.

Katika ufunguzi huo, Mheshimiwa Makame amesisitiza kuwa sekta ya kilimo ndiyo mhimili mkuu wa uchumi wa mkoa, hivyo jukwaa hilo linafungua ukurasa mpya wa mipango shirikishi itakayowezesha mkoa kuongeza uzalishaji, uongezaji wa thamani na masoko ya uhakika.

Katika jukwaa hilo, washiriki wanatarajiwa kujadili kwa kina hali ya sekta ya kilimo katika Mkoa wa Songwe, ikijumuisha fursa zilizopo, changamoto zinazowakabili wakulima pamoja na hatua zinazohitajika ili kuongeza tija katika uzalishaji. Aidha, tathmini ya uzalishaji wa mwaka 2025 pamoja na mpango wa uzalishaji wa mwaka 2026 itawasilishwa, sambamba na maandalizi ya msimu ujao wa kilimo kwa mwaka 2026 ili kuhakikisha mkoa unaendelea kuwa kinara katika uzalishaji wa mazao ya kimkakati.

Vilevile, jukwaa litajadili masuala yahusuyo usindikaji wa mazao, uongezaji wa thamani, biashara, masoko pamoja na upatikanaji wa mitaji, ambapo wadau mbalimbali wataeleza namna mnyororo wa thamani wa mazao unavyoweza kuimarishwa ili kumpa mkulima kipato zaidi. Kadhalika, mada kuhusu kilimo hifadhi na mikakati ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi itazungumziwa, ikilenga kuwajengea wakulima uelewa wa matumizi ya mbinu rafiki kwa mazingira na kuhimili athari za mabadiliko ya hali ya hewa.

Mkuu wa Mkoa amehimiza wadau wote kutumia jukwaa hilo kama chombo cha kuweka mikakati thabiti ya kubadilisha sekta ya kilimo kuwa ya kisasa na yenye ushindani, ili kuongeza kipato cha wananchi na kuchangia ukuaji wa uchumi wa mkoa wa Songwe.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MAKAME AONGOZA JUKWA LA WADAU WA KILIMO MKOANI SONGWE.

    November 19, 2025
  • RC CHONGOLO AONGOZA KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI WILAYA YA MOMBA KUJADILI HOJA ZA CAG

    June 11, 2025
  • RC CHONGOLO AONGOZA KIKAO CHA KUJADILI HOJA ZILIZO BAINISHWA KATIKA RIPOTI YA CAG HALMASHAURI YA MBOZI

    June 10, 2025
  • RC CHONGOLO APIONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA ILEJE KWA KUPATA HATI SAFI

    June 10, 2025
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.