• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC MGUMBA AMUONYA AFISA ELIMU SEKONDARI KWA KUMDANGANYA.MBOZI:

Posted on: June 7th, 2022

RC MGUMBA AMUONYA AFISA ELIMU SEKONDARI KWA KUMDANGANYA.MBOZI: 

Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Omary Mgumba amemuonya Afisa Elimu Sekondari Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi kwa kumudanganya juu ya ujenzi wa Sekondari ya Ichenjezya.Afisa Elimu Sekondari alimudanganya Mkuu wa Mkoa wakati akiwa kwenye ziara ya ukaguzi wa miradi katika Sekondari ya Senye iliyopo Kata ya Vwawa baada ya Mkuu wa Mkoa kuhoji sababu iliyosababisha Halmashauri kujenga Sekondari Kata ya Vwawa na kuacha kujenga Kata ya Ichenjezya ambayo haina Sekondari na muongozo wa unataka kipaombele cha kwanza Shule ikajengwe kwenye Kata ambayo haina Sekondari.Mkuu wa Mkoa alipomuuliza kwa nini hawajajenga Kata ya Ichenjezya, Afisa Elimu akasema hawajajenga kwa sababu Ichenjezya wana eneo dogo la ekari 4, eneo ni oevu, maji yanajaa katika eneo ilo, watalamu walisema eneo halifai, eneo liko Kata ya Hasanga na sio Ichenjezya mwisho wasingeweza kupeleka fedha za Serikali kwenye ujenzi Sekondari kwa sababu izo.Baada ya Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Omary Mgumba kukatisha ziara yake na kuamua kwenda Kata ya Ichenjezya na kujionea hali halisi akakuta taarifa aliyopewa na Afisa Elimu Sekondari ni tofauti na uhalisia uliopo.Mkuu wa Mkoa amekuta eneo la Shule ya Sekondari lina ekari 8, maboma ya shule yamejengwa tangu 2019 na Halmashauri imepeleka fedha takribani Milioni 10 pamoja na wadau wengine wamechangia.Kufuatia hali iyo, Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Omary Mgumba ameuagiza Uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi kuhakikisha wanafanya jitihada za kukamilisha Sekondari ya Ichenjezya ili ianze kufanya kazi.Tusiwaachie wananchi peke yako katika ujenzi huu Halmashauri ongezeni nguvu ili mradi huu uishe haraka.Diwani viti maalumu Tarafa ya Vwawa, Mhe. Neema Nzowa amemshukuru Mkuu wa Mkoa Kwa ziara yake na amemuomba asaidie kufanikisha ukamilishaji wa Shule.Diwani wa Kata ya Ichenjezya, Mhe. Bahati Mbughi amesema walipolibaini eneo waliwaita watalamu na wakasema linafaa kujenga Shule na tukaletewa ramani ya Shule na Halmashauri ilimtuma injinia kuja kusimamia ujenzi wa msingi.Wananchi wamechangia nguvu kazi za thamani ya shilingi Milioni 13 na wametoa ushirikiano wa kutosha katika ujenzi na wao ndio wamekuwa wakichota maji na shughuli nyingine za ujenzi kama kuchanganya zege.Mtendaji wa Kata ya Ichenjezya, Bi. Atupakisye Malakalinga amesema hadi sasa nguvu za wananchi ni Milioni 13.6, Halmashauri imeleta Milioni 10 pamoja na bati 270, mfuko wa jimbo bati 54 na saruji 104, Mbunge wa Jimbo la Vwawa mifuko 25 ya saruji na Kamati ya elimu  210,000.Malengo yetu ni ifikapo januari 2023 Shule ianze kufanya kazi kutokana na wananchi wanamuitikio mzuri.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.