• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC MGUMBA ATOA SIKU 7 HUDUMA ZA MAMA NA MTOTO ZIANZE KUTOLEWA HOSPITALI YA RUFA

Posted on: June 2nd, 2022

RC MGUMBA  ATOA SIKU 7 HUDUMA ZA MAMA NA MTOTO ZIANZE KUTOLEWA HOSPITALI YA RUFA

SONGWE: Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Omary Mgumba ametoa siku saba kwa uongozi wa Hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Songwe kuanza kutoa huduma ya mama na mtoto katika hospitali mpya ya rufaa iliyopo Hasamba.

Mkuu wa Mkoa ametoa agizo hilo alipofanya ziara ya ukaguzi wa shughuli za ujenzi pamoja na huduma katika Hospitali mpya ya rufaa ya Mkoa, 2 Juni 2022.

Mkuu wa Mkoa amesema anataka kuona huduma ya Mama na mtoto zinaanza haraka ndani ya siku saba na watalamu wote wa afya wa ngazi ya Mkoa wahamia mara moja katika Hospitali mpya ya rufaa ya Mkoa ili Serikali ijue mapungufu yaliyopo katika Hospitali ya Vwawa  na kutatua haraka kabla ya kufika Julai 2022.

 “Halmashauri ya Mbozi imetufadhili Mkoa vya kutosha ni muda sasa Mkoa kuhamia katiak Hospitali hii na serikali ione upungufu uliopo katika Hospitali ya Vwawa  na kushugulikia mapungufu  ” Mhe. Omary Mgumba.

Kaimu Mkurugenzi  wa Hospitali ya Mkoa, Dkt Ahmed Ramadhan amesema hadi sasa wagonjwa 1,163 wamepata huduma kwa upande wa wagonjwa wa nje tu na wagonjwa 12 wamepata huduma ya kulazwa.

Ingawa wodi hazijakamilika ziko kwenye ujenzi, lakini uongozi wa Hospitali tuliamua kutenga baadhi ya vyumba kwenye jingo la wagonjwa wa nje na kuvigeuza wodi kwa wale wagonjwa ambao watahitajika kulazwa, amesema Dkt. Ahmed.

Aidha, Dkt. Ahmed amesema ifikapo Julai 2022 baada  kukamilisha  jengo la  wagonjwa  wa dharura na maututi huduma kwa watoto njiti ambao wamezaliwa kabla ya miezi tisa kufika pamoja na kutoa huduma kwa wagonjwa wa dharura zitaanza kutolewa.

“Watoto wanaozaliwa kabla ya miezi tisa tumekuwa tunawapeleka Mkoa wa Mbeya pamoja na wale wagonjwa maututi nah ii ni kutokana Mkoa wa Songwe tulikuwa hatuna miundombinu ya kuwahudumia lakini kwa sasa majengo haya ya wagonjwa maututi na dharura kukamilika wagonjwa watapata huduma hapa hapa” Dkt. Ahmed.

Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Omary Mgumba amesema ndani ya mwaka mmoja Rais Samia Suluh Hassan ameleta fedha zaidi ya shilingi Bilioni 8.5 katika Hospitali ya Mkoa tu kwa ajili ya ukamilishaji wa jengo la wagonjwa wa nje, ujenzi wa jengo la mama na mtoto, jengo la dharura na maututi pamoja na nyumba ya mtumishi.

Mkuu wa Mkoa ameuagiza uongozi wa Hospitali kukamilisha  majengo ya dharura, maututi na nyumba ya mtumishi  kabala ya kufika Julai 2022 na jengo la wodi za mama na mtoto lilamilike kabla ya kufika oktoba 2022 na kumtaka mkandarasi kufanya kazi usiku na mchana.

Wakati huo huo  Mkuu wa Mkoa  ameuagiza uongozi wa Hospitali wakati majengo yanakamilishwa na vifaa tiba vyote ambavyo vimeagizwa navyo viwe vimefika kabla ya kufika Julai 2022 na huduma zianze haraka.

MWISHO

 

 

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.