• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC MGUMBA AWATOA HOFU WAMACHINGA UJENZI WA SOKO TUNDUMA.SONGWE

Posted on: May 26th, 2022

RC MGUMBA AWATOA HOFU WAMACHINGA UJENZI WA SOKO TUNDUMA.SONGWE: Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Omary Mgumba amewatoa hofu wamachinga ambao watakosa eneo katika ujenzi wa soko linaloendelea la majengo katika mji wa Tunduma.Mkuu wa Mkoa amesema Serikali itaendelea kujenga masoko lengo ni kuhakikisha kila mfanyabiashara mdogo anapata sehemu nzuri ya kufanyika kazi katika masoko rasmi na kutatua changamoto za wamachinga.Mkuu wa Mkoa amesema hayo alipokutana na viongozi wa shirikisho la wamachinga Mkoa wa Songwe ofisini leo Mei 26."soko la majengo ni mwanzo tu, likimalizika Serikali itajenga na lingine hatutaki kujenga masoko mengi kwa wakati moja alafu tushindwe kumaliza na kubaki magofu tunataka tukianza kujenga na tunamaliza moja kwa moja" amesema  Mhe. Omary Mgumba.Aidha, Mkuu wa Mkoa amesema wakati ujenzi wa soko la mejengo unaendelea, pia tunaendelea kukamilisha stendi ya Mpemba ambayo tayari kuna eneo maalumu kwa wamachinga, eneo maalumu kwa minada hivyo kila machinga atapata fursa ya kufanya biashara.Pia kuhusu madereva wa malori Mkuu wa Mkoa amesema nao wanatengewa sehemu maalumu karibu na sehemu wanakopaki magari yao kwa ajili ya kununua bidhaa mbalimbali ili watakapokuwa wamepaki wanajua sehemu fulani anakwemda kununua bidhaa na sio barabarani tu.Mkuu wa Mkoa ametoa wito kwa wamachinga kutofanya biashara barabarani kutokana na hatarii zilizopo za ajali, matukio ya moto pamoja na kutofanya biashara mbele ya Nyumba ya mtu.Kwa upande wao viongozi wa shirikisho la wamachinga Mkoa wa Songwe wameishukuru Serikali ya Rais Samia Suluh Hassan kwa kuwajali kwa vitendo kwa kutoa fedha Milioni 10 kwa kila Mkoa kwa ajili ya kuimarisha shirikisho la wamachinga na wamachinga.Katibu wa Shirikisho la wamachinga Mkoa wa Songwe, Judith Msemwa amesema lengo la shirikisho ni kutoa elimu kwa wamachinga wanaotembea ili angalau awe Kuna sehemu ambayo Serikali inamtambua na aweze kunufaika na fursa zinazotoka Serikali kama mkopo.Mwenyekiti wa Shirikisho la wamachinga Mkoa wa Songwe, Kelvin Kyando amesema tunataka wamachinga wawe wazalendo kwa nchi yao ikiwa ni pamoja na kujitokeza kwenye baadhi ya shughuli za umma na kuchangia baadhi ya ushuru kwa Halmashauri ambao ni rafiki kwa wamachinga.Elizabeth Mwasandube ambaye ni mfanyabiashara maarufu kama machinga amesema kwa sasa Serikali inafanya kazi kwa karibu na ushirikiano na viongozi wa machinga na hakuna manyanyaso.MWISHO

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.