• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC MWANGELA AINGIA MKATABA NA WAKUU WA WILAYA KUHUSU USAFI WA MAZINGIRA

Posted on: April 23rd, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brig. Jen. Nicodemus Mwangela leo ameingia mkataba na wakuu wa Wilaya zote nne za Mkoa wa Songwe kwa ajili ya utendaji kazi na usimamizi wa Huduma za Maji na Usafi wa Mazingira.

Mara baada ya kusaini mikataba hiyo Brig. Jen, Mwangela amewaeleza kuwa mkataba huo uanze kuonyesha mabadiliko ndani ya miezi sita ili baada ya miaka minne ya mkataba kumalizika kila wilaya iwe na mazingira safi ikiwa ni pamoja na kila mwananchi kuwa na choo bora.

Amesema katika kutekeleza mkataba huo shirika la UNICEF wameahidi kushirikiana na Mkoa wa Songwe ili kufikia malengo  kwani wameona nia na mipango madhubuti ya kuhakikisha usafi wa mazingira unakuwa kipaumbele kwa mkoa wa Songwe.

“Katika kutekeleza mkataba huu nitakuwa nawapima wakuu wa Wilaya kwa kutumia vigezo vilivyoandaliwa na wataalamu ili tujue nani anafanya vizuri, nitapita katika vijiji tena kwa kushtukiza, nitakagua nyumba za viongozi wa vijiji, sokoni, shuleni na nitaongea na kamati zilizoundwa nitapima na nitatoka na majibu”, amesema Brig. Jen. Mwangela.

Brig. Jen. Mwangela ameongeza kuwa suala la usafi linazuia magonjwa mengi ambayo yanaweza kuepukika huku akielekeza  ifikapo mwisho wa mwaka huu kila halmashauri ihakikishe kuna vijiji ishirini vya mfano vyenye vyoo bora na vinazingatia usafi wa mazingira.

Katibu Tawala Mkoa wa Songwe Dkt Seif Shekalage amesema mkataba huo umewekwa ikiwa ni siku chache baada ya timu ya Mkoa kufanya ziara Mkoani Njombe na kujifunza utekelezaji wa Kampeni ya Usafi wa Mazingira hivyo viongozi wote wana elimu ya kutosha.

Dkt Shekalage amesema mara baada ya Mkataba huo kusainiwa wakurugenzi wafikishe ujumbe wa usafi wa mazingira kwa watendaji wa Halmashauri ili kila mmoja atimize wajibu wake.

Akizungumza kwa niaba ya Wakuu wa Wilaya za Mbozi, Songwe  na Ileje  Mkuu wa Wilaya ya Momba Juma Irando amesema wao wako tayari kushirikiana na kila anayehusika ili kufanikisha kampeni ya usafi wa mazingira na wako tayari kwa kazi.

Irando ameongeza kuwa wanamuunga mkono Mkuu wa Mkoa na wako tayari kujitoa ili kufanikisha hilo huku akiwashukuru UNICEF kwa ushirikiano ili kuhakikisha Mkoa wote wa Songwe unafanikiwa katika masuala ya usafi wa mazingira.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.