• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC SONGWE ATOA SULUHU MGOGORO WA UCHIMBAJI MADINI

Posted on: November 12th, 2018

  Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brig. Jen. Nicodemus E. Mwangela akiwa na kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wamesuluhisha mgogoro baina ya wakazi wawili wa kijiji cha Saza Wilaya ya Songwe kuhusu eneo la uchimbaji wa madini.

Brig. Jen. Mwangela amesema Suzan Karan amebainika kisheria kuwa ni mmiliki halali wa eneo lililokuwa likigombewa kwa kuwa ana leseni halali huku Elimbotwa Naftari ambaye hana leseni na amekuwa akidai umiliki wa eneo hilo amebainika kuendesha shughuli za uchimbali kinyume na sheria.

“Sheria inamtambua Suzan kama mmliki halaki kwakuwa anayo leseni na amefuata taratibu na sheria za uchimbaji madini, tunashauri Elimbotwa kama atataka kuendelea kuchimba madini katika eneo hilo basi akubaliane na Suzan kufanya naye kazi”, amesisitiza.

Ameongeza kuwa serikali za vijiji hazina mamlaka ya kuwapa vibali vya uchimbaji wawekezaji wa madini bali leseni na vibali vyote vya uchimbaji wa madini hutolewa na ofisi za madini Wilaya, mkoa au kanda, hii inatokana na kuwa serikali ya kijiji ilimtambua Elimbotwa kama mmiliki wa eneo la uchimbaji kinyume na sheria.

Kwa upande wake Elimbotwa amesema anamtambua Suzan kama mmliki halali wa eneo walilokuwa wakiligombania isipokuwa sasa anadai fidia ya zaidi ya shilingi milioni 190 ikiwa ni gharama ya vitu alivyowekeza kabla ya Suzan kupewa leseni ya eneo hilo.

Naye Suzan ameupongeza uongozi wa Mkoa kwa kutoa suluhu ya mgogoro huo kutokana na kuwa ulipelekea kusimama kwa shughuli za uchimbaji na hivyo kuathiri uchumi wake.

Aidha Brig. Jen. Mwangela ameagiza Takukuru, TRA na taasisi zinazoweza kufanya ukaguzi, zihakiki madai ya Elimbotwa kama ni halisi ili Suzan aweze kuyalipa.

Imeelezwa kuwa baadhi ya migogoro ya haki ya kumiliki maeneo ya uchimbaji wa madini mkoani Songwe inasababishwa na ukiukwaji wa taratibu na sheria za madini unaofanywa na baadhi ya watendaji na wachimbaji.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.