• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

SENEDA: AZITAKA HALMASHAURI KUWEKA RATIBA YA KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI

Posted on: August 10th, 2022

SENEDA: AZITAKA HALMASHAURI KUWEKA RATIBA YA KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI

SONGWE: Katibu Tawala Mkoa wa Songwe, Bi. Happiness Seneda amezitaka Halmashauri zote za Mkoa wa Songwe kuweka ratiba ya wazi kwa wananchi ya kusikiliza kero zao.

Katibu Tawala Mkoa ametoa maagizo hayo Agosti 10, alipokutana na watumishi wa Halmashauri ya Mji Tunduma na Halmashauri ya Mbozi kwa lengo la kufahamiana baada ya kuhamia Mkoa wa Songwe akitokea Mkoa wa Iringa.

Bi. Happiness Seneda amesema anataka kuona ratiba ya wazi inayofahamika kwa wananchi na iwekwe kwenye mbao za matangazo, tovuti na sehemu yeyote ambayo wananchi wanaweza kuiona ili wajue ni siku gani Halmashauri yao inasikiliza kero zao.

"Nataka kuona timu ya kusikiliza kero ipo au mtu maalumu wa kusikiliza kero na nijue ni lini kero za wananchi zinasikilizwa na ziwe kwenye kumbukumbu na nione wananchi wanapata mrejesho wa kero walizowasiliaha" Bi. Happiness Seneda

Katibu Tawala Mkoa, amesema hataki kuona mwananchi amewasilisha kero yake na inachukuliwa kawaida tu, anahitaji kuona kero yake inasikilizwa hadi mwisho na apate mrejesho wa kero yake.

Halmashauri zote zikitimiza wajibu wao wa kusikiliza kero za wananchi basi kero hizo haziwezi kufika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwani Mkoa haumiliki ardhi au wananchi bali wote wako chini ya Halmashauri husika, amesema Katibu Tawala Mkoa wa Songwe, Bi. Happiness Seneda.

Pamoja na kusikiliza kero za wananchi Pia, Katibu Tawala Mkoa Songwe, Bi. Happiness Seneda amezielekeza Halmashauri kusikiliza kero na changamoto za watumishi ili kujua watumishi wake wanakumbana na changamoto zipi.

Haipendezi mtumishi yuko hapa ana kero na changamoto nyingi lakini sisi kwa sisi watumishi tunashindwa kuzitatua, hii haikubaliki.

Wakati huo huo ameziagiza Idara ya elimu na afya ambazo ndio zina watumishi wengi kuwatembelea watumishi wao na kutatua kero zinazowakabili na kuwatia moyo juu ya ufanyaji kazi.

MWISHO.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.