• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

Posted on: March 20th, 2025

Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), Mkuu wa Mkoa wa Songwe Mhe. Daniel Chongolo , Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso wameshuhudia utiwaji saini wa Mkataba wa Ujenzi wa Mradi wa Maji wa Tunduma,- Vwawa, Kati ya Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Eng. Mwajuma Waziri, kwa niaba ya Serikali na Meneja Mradi wa Kampuni ya Ukandarasi ya China (China Civil Engineering Construction Corporation-CCECC), Bw. Ning Yunfeng,





Tukio hilo limefanyika katika Uwanja wa Shule ya Msingi Tunduma leo tarehe 20 Machi 2025 ambapo mradi huo kutoka Chanzo cha Maji ya Mto Momba, uliopo Wilaya ya Momba, mkoani Songwe utakaogharimu shilingi bilioni 119.9 za Tanzania.


Akizungumza Mhe. Chongolo amesema Mradi huo utahusisha ujenzi wa chanzo cha maji (Intake) chenye uwezo wa kuhifadhi lita milioni 21.5, ujenzi wa Kituo cha kuchakata na kutibu maji chenye uwezo wa kuzalisha lita 20m kwa siku, ujenzi wa mtandao wa mabomba ya kusafirisha maji yenye kipenyo cha 100mm yenye urefu wa kilometa 96, ujenzi wa matenki ya maji yenye uwezo wa kuhifadhi ujazo wa lita 5m  litakalojengwa katika Mtaa wa Uwanjani/Uhuru, Hakmashauri ya Mji-Tunduma, tenki la lita 3m litakalojengwa katika Kijiji cha Ikana na tenki lenye ujazo wa  lita 2m litakalojengwa katika Kijiji cha Nkangamo, Ununuzi wa pampu, Ujenzi wa Ofisi na Vitendeakazi vingine.


Akihutubia mamia ya wakazi wa Mkoa wa Songwe waliojitikeza kushuhudia tukio hilo katika Viwanja vya Uwanjani, mjini Tunduma, Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, aliwahakikishia wananchi hao kuwa Serikali itatoa fedha zote za kutekeleza mradi huo ambao ni ahadi ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ya kumtua mama ndoo kichwani.


Kwa upande wake, Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso, alimpongeza Mhe. Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kutoa kiasi hicho cha fedha takriben sh. bilioni 120, ambazo ni fedha za ndani, kwa ajili ya kuwaondolea adha ya maji wananchi wa Tunduma, Vwawa na Mlowo, watakaofikiwa na mradi huo.


Mradi huo unatarajia kuwanufaisha wakazi 219,309 katika miji hiyo ya Tunduma, Vwawa na Mlowo, ambapo ujenzi wake utachukua miezi 18 kukamilika na kuanza kutoa maji safi na salama.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.