Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Jabiri Omari Makame, leo tarehe 07 Februari 2026 amefanya utambulisho wa mfumo wa kidijitali unaojulikana kama “Songwe Serikali Kiganjani”, mfumo unaolenga kusogeza huduma za Serikali karibu zaidi na wananchi kwa njia ya teknolojia ya kidijitali.
Akizungumza wakati wa tukio hilo lililofanyika katika Ukumbi wa Kanisa la Moravian, Vwawa, wilayani Mbozi, Mhe. Makame amesema kuwa mfumo huo ni sehemu ya utekelezaji wa ahadi za siku mia moja (100) za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kuimarisha matumizi ya TEHAMA ndani ya Serikali na kuongeza uwazi, uwajibikaji pamoja na ufanisi katika utoaji wa huduma kwa wananchi.
Ameeleza kuwa kupitia mfumo wa “Songwe Serikali Kiganjani”, wananchi wataweza kupata taarifa muhimu za Serikali, kufuatilia huduma mbalimbali pamoja na kutoa maoni na mapendekezo yao kwa urahisi zaidi, hatua itakayosaidia kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali na wananchi.
![]() |
![]() |
![]() |
Mhe. Makame amewataka wananchi wa Mkoa wa Songwe kuutumia mfumo huo ipasavyo ili kunufaika na fursa za kidijitali zinazotolewa na Serikali, akisisitiza kuwa hatua hiyo ni uthibitisho wa dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kuwaletea wananchi maendeleo kwa vitendo.
Kwa ujumla, utambulisho wa mfumo wa “Songwe Serikali Kiganjani” unaonesha wazi kuwa Serikali inaendelea kutekeleza ahadi zake kwa wananchi.
2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi
Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE
Simu: 025 2580305
Simu ya Kiganjani: 025 2580305
Barua pepe: ras@songwe.go.tz
Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.