• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

SONGWE KUUNDA KIKOSI KAZI KUONGEZA WANACHAMA WA CHF

Posted on: November 17th, 2020

SONGWE KUUNDA KIKOSI KAZI KUONGEZA WANACHAMA WA CHF

Uongozi wa Mkoa wa Songwe umejipanga kuunda kikosi kazi cha kuhamasisha makundi mbalimbali ya jamii kama vile Bodaboda, Mama ntilie, waliopo  kwenye vyama kama SACOS pamoja na makundi mengine kujiunga na Bima ya Afya ya Jamii iliyoboreshwa (CHF) hili kuweza kuongeza wanachama zaidi 25% kutoka 1.6% iliyopo sasa ifikapo Disemba 2020.

Hayo yamebainishwa na Katibu Tawala Mkoa wa Songwe, Dr. Self Shekalaghe wakati wa kikao kazi na watumishi  wanaohusika na uandikishaji wa CHF iliyoboreshwa, wadau wa Afya, Makatibu wa Afya pamoja na Waganga wakuu wa Halmashauri kilichofanyika ukumbi wa Vwawa Sekondari, 17 Novemba 2020.

Katibu Tawala Mkoa wa Songwe, Dr. Self Shekalaghe amesema kwa sasa Mkoa kitaifa uko nafasi ya 24 katika uandikishaji wa CHF na tumefika 1.6% tu sawa na Kaya 3,300 ambazo zimeandikishwa wakati lengo la Kitaifa ni kila Mkoa ufike 30% ya kuandikisha wanachama wa CHF. 

“Pamoja na kuunda kikosi kazi cha kuhamasisha makundi mbalimbali tunatafuta wadau mbalimbali waweze kutusaidia kufikia lengo kama ambavyo shirika la HIMSO limetusaidia usafiri wa Pikipiki ambazo watapewa waratibu kila Wilaya hili kuhakikisha uandikishaji wa wanachama wa CHF  unaongezeka” Katibu Tawala Mkoa, Dr. Shekalaghe.

Katika kuongeza asilimia za wanachama wa CHF Shirika la HIMSO limechangia pikipiki 4 zenye thamani ya shilingi Milioni 27.1 kwa ajili ya Halmashauri ya Songwe, Ileje, Momba na Tunduma.

Wakati huo huo Katibu Tawala wa Mkoa, Dr. Shekalaghe amesema  pikipiki zilizotolewa na Shirika la HIMSO atazigawa kwa Halmashauri husika baada ya kutimiza malengo ambayo watawekeana ya uandikishaji wa wanachama wa CHF kwa muda wa wiki 2 ndio watapewa kwa waliotimiza malengo tu.

Kujiunga na CHF kwa kaya ni Shilingi 30,000 ambayo utaweza kutibiwa katika Zahanati, Vituo vya Afya, Hospitali za Wilaya pamoja na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ndani ya Mkoa wa Songwe tu.

Ikumbukwe Katika CHF ya zamani kufikia Desemba 2018 Mkoa wa Songwe umekuwa kinara kitaifa kwa 76.4% na kufanikisha kaya 198,376 kujiunga na CHF ya zamani

 

   

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.