• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

SONGWE YAKAMILISHA MAANDALIZI YA SENSA KWA 96%

Posted on: August 19th, 2022

SONGWE YAKAMILISHA MAANDALIZI YA SENSA KWA 96%

SONGWE: Zikiwa zimebaki siku 4 zoezi la Sensa ya watu na makazi kufanyika, Mkoa wa Songwe umekamilisha maandalizi yote na kazi imebaki kwa wananchi kuhesabiwa tu.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Wilaya ya Mbozi, Mhe. Cosmas Nshenye wakati akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Songwe kweye kikao cha Kamati ya Sensa Mkoa kilichofanyika leo Agosti 19.

Mhe. Cosmas Nshenye ametoa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Songwe kujitokeza kwa wingi na kutoa ushirikiano kwa makalani wa Sensa ambao watapita kwenye Makazi yao kwa ajili ya kupata taarifa sahihi za Sensa.

Pia, Mhe. Cosmas Nshenye ametoa wito kwa viongozi wa Serikali kuanzia ngazi ya kitongoji hadi Mkoa kutoa ushirikiano wa hali na Mali kwa makarani watakapokuja wanapita kwenye Makazi yao ili kufanikisha zoezi la Sensa ya watu na makazi.

Mratibu wa Sensa Mkoa, Ndg. Doto Ibrahim amesema makalani wako tayari kwa kazi ya Kuhesabu watu na makazi kuanzia tarehe 23 Agosti 2022.

Tunajua kabisa Mkoa wetu unapakana na nchi ya Malawi na Zambia ambao wanaingia kufanya shughuli mbalimbali za kiuchumi, hivyo nasi tumejipanga katika maeneo yote ambayo wageni wanafikia ikiwa ni pamoja na sehemu za maegesho ya magari ya Malori ili kuhakikisha wote wanahesabiwa, amesema Doto Ibrahim mratibu wa Sensa Mkoa.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Songwe, Bi. Happiness Seneda amesema Serikali imejipanga vizuri kuhakikisha kila mtu anahesabiwa ata kama sehemu iyo kuna migogoro ya mipaka hayawezi kuathiri zoezi la Sensa kwani Sensa ya 2022 inafanywa Kidigitali zaidi.

Pia, ametoa wito kwa wanawake kutoa ushirikiano mzuri kwa makalani kwenye kipengele cha maswali ya uzazi, kwani eneo ilo anapaswa kujibu mwanamke na sio mwanaume, hivyo tunahitaji ushirikiano.

Sheikh wa Mkoa wa Songwe, Sheikh Hussein Batuza ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Amani Mkoa ametoa wito kwa waumini wa dini ya kiislamu na wananchi wote wa Songwe kumuunga mkono kwa vitendo Rais wa Tanzania, Mhe. Samia Suluh Hassan kufanikisha zoezi la Sensa ya watu na makazi.

Sensa ya 2022 itakuwa ya kwanza kwa Mkoa wa Songwe tangu uanzishwe 2016 na ni ya sita kwa nchi nzima.

MWISHO.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.