• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

SONGWE YAPANIA KUONGOZA KITAIFA USAFI WA MAZINGIRA

Posted on: April 21st, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brig. Jen. Nicodemus Mwangela amesema muda si mrefu Songwe itakuwa kinara katika  kutekeleza kampeni ya usafi wa mazingira kwani sasa utekelezaji wa kampeni hiyo unaenda kufanyika kwa kasi na ufanisi mkubwa.

Brig. Jen. Mwangela ameyasema hayo mara baada ya kutembelea vijiji  vya Halmshauri ya Wilaya ya Njombe ikiwa ni sehemu ya ziara ya kuona namna walivyotekeleza Kampeni ya Usafi wa Mazingira kwa ufanisi na kuongeza kuwa sasa amebaini siri ya mafanikio yao.

“Nimeona na nimejua siri yao na sasa tumejifunza mengi tunaenda kutekeleza kampeni hii kwa kasi kubwa, tutawashirikisha tuwape elimu wananchi,  viongozi wa dini  na wa serikali ngazi zote, kila mmoja aweze kuhusika kikamilifu ili wote tuibebe kwa pamoja kampeni hii.”, amesema Brig. Jen. Mwangela.

Ameongeza kuwa katika kutekeleza kampeniya usafi wa mazingira kwa ufanisi watahakikisha wale wasio na uwezo na hawana ndugu wanawekewa utaratibu wa kusaidiwa na uongozi wa vijiji na mitaa ili kila kaya iwe na choo bora na kuweka sheria ili kuwabana wachache watakao kaidi.

Brig. Jen. Mwangela ameongeza kuwa si kwamba Mkoa wa Songwe unafanya vibaya sana katika usafi wa mazingira bali utekelezaji wa kampeni hii unapaswa kufanyika kwa kasi zaidi na ufanisi mkubwa pia ameomba ushirikiano wa wananchi wote waichukue kampeni kwa uzito mkubwa.

Katibu Tawala Mkoa wa Songwe Dkt Seif Shekalaghe amesema kampeni ya usafi wa mazingira ni ajenda ya kitaifa ambayo ina mipango mikakati inayotumika maeneo yote hivyo wamefanya ziara kujionea namna Mkoa wa Njombe ambao unafanya vizuri kitaifa umetekelezaje mipango hiyo.

Dkt Shekalaghe amesema wamejifunza kuwa Njombe wamefanikiwa kwakuwa walitekeleza kampeni ya usafi wa mazingira kwa ushirikiano mkubwa kuanzia ngazi ya chini, elimu ilitolewa kwa watu wote wakaielewa na kuitekeleza vizuri, kujitoa kwa viongozi pamoja na wananchi kujiwekea sheria ndogo ndogo zinazo elekeza faini kwa wanao kaidi.

Naye Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Matiganjola Wilayani Njombe Erasto Joseph Kapinga amemuambia Mkuu wa Mkoa wa Songwe kuwa wana kijiji wote walipewa elimu ya usafi wa mazingira  na mafanikio ya kampeni hiyo ni pamoja na kutokuwepo kwa magonjwa ya tumbo na kuharisha kijijini hapo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.