• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

SONGWE YAPONGEZWA KWA KUSIMAMIA AGIZO LA WAZIRI MKUU KATIKA ZAO LA KAHAWA.

Posted on: March 5th, 2018

  Naibu Waziri Kilimo Dkt Mary Mwanjelwa ameupongeza uongozi wa Mkoa wa Songwe kwa kusimamia vema agizo la Waziri Mkuu la kutaka Kahawa kutonunuliwa kwa wakulima bali uuzaji ufanyike katika minada kwa kupitia vyama vya ushirika.

Dkt Mwanjelwa ametoa pongezi hizo mapema jana alipofanya ziara Mkoani hapa na kuzungumza na uongozi wa Mkoa, wakulima na wanunuzi wa kahawa ambapo ameeleza kuwa jitihada za Mkoa wa Songwe zimeonyesha kuunga mkono serikali  ya awamu ya tano kwa vitendo.

“Taarifa yenu inaonyesha ongezeko la vyama vya ushirika 17 tangu Waziri Mkuu atoe malekezo hayo mwezi Januari, jitihada hizi zinaonyesha mnaunga mkono jitihada za serikali ya awamu ya tano ya kumkomboa mkulima na mwananchi wa hali ya chini kwa vitendo”, ameeleza Dkt Mwanjelwa.

Ameongeza kuwa elimu juu ya ushirika itolewe kwa wakulima ili wote wajiunge na kuacha kuuza kahawa yao kwa madalali ambao wamekuwa wakiwapunja na hivyo kudhoofisha kilimo cha kahawa.

Dkt Mwanjelwa ameeleza kuwa Wizara yake itaendelea kusimamia na kuhakikisha kuwa mbolea inawafikia wakulima kwa wakati huku akiwataka watendaji kuzingatia maelekezo ya serikali katika usambazaji wa mbolea.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Songwe Chiku Gallawa ameeleza kuwa mkoa unahakikisha Mkulima wa kahawa anafaidika na kilimo hicho kwa kumuelimisha ajiunge na ushirika ili kuepuka madalali ambao wamekuwa wakiwadhulumu.

Gallawa ameeleza kuwa wakulima waliokuwa wamejiunga katika vikundi wataelekezwa namna ya kujiunga katika ushirika ili kutoruhusu watu wachache kufaidi jasho la Mkulima ambaye ndiye mlengwa wa kilimo cha kahawa.

Nao wakulima wa kahawa wa Kijiji cha Isansa Wilaya ya Mbozi wamemueleza Naibu Waziri Dkt Mwanjelwa kuwa wanaunga mkono kauli ya Serikali ya kujiunga katika ushirika kwakuwa wamekuwa wakidhulumiwa na madalali wa zao hilo la kahawa.

Aidha wameitaka serikali kutorudi nyuma katika uamuzi huo wa kuwataka wajiunge katika ushirika huku wakiomba ushirika uboreshwe zaidi ili kuondoa changamoto zilizokuwepo hapo zamani.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.