• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

UMASIKINI WATAJWA CHANZO CHA UKATILI KWENYE FAMILIA.

Posted on: May 15th, 2022

UMASIKINI WATAJWA CHANZO CHA UKATILI KWENYE FAMILIA.

SONGWE: Familia zimehimizwa kufanya kazi kwa bidii na kupambana na umasikini uliopo hili kuepuka ukatili wa kiuchumi na Kijinsia ambao umekuwa ukishamiri kwenye familia nyingi. 

Wito huo umetolewa na wajumbe wa kongamano la familia wakati wa wakiadhimisha siku ya Familia Duniani ambalo limefanyika Wilaya ya Mbozi, 15 Mei 2022.

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Songwe, Ndg. Elynico Mkola amesema ni vizuri jamii na Serikali kusisitiza kwa nguvu zote watu wafanye kazi hili wapate kipato cha kuhudumia familia zao.

Mkola amesema ata jamii kwa sasa imebadilika inaona Mafanikio ni kitu ambacho kina kuja kwa muda mfupi na sio kufanya kazi. 

"Mwanaume kama unaweza kuitunza familia yako hakuna mwanamke mwenye kibuli hivyo hivyo kwa mwanamke ukifanya kazi na ukaweza kumudu familia huwezi kupata ukatili wa aina yeyote kutoka kwa mwanaume,  kwani hakuna mwanaume anayedharua mwanamke mwenye fedha" Elynico Mkola.

Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Omary Mgumba ametoa wito kwa familia kukaa pamoja na kujadili namna ya kufanya kazi kwa manufaa ya familia zao.

"Tusivutane mashati kwenye familia kila mmoja ndani ya familia afanye kazi hili kila mtu aweze kujimudu na kuogopa kuwa kupe" Mhe. Omary Mgumba.

Aidhaa, Mkuu wa Mkoa ametoa wito kwa jamii na familia kutokuwa chanzo kwa vitendo viovu kwa kusifia na kushabikia mtu mwizi wa mali za umma hili tuweze kuisadia Taifa na familia.

Pia, ametoa wito kwa akinamama haswa wale ambao wanafanya kazi kuacha ukatili wa kiuchumi kwa wanaume zao kwa madai mshahara wa mwanamke ni wake tu lakini mshahara wa mwanaume ni wao wote jambo ambalo ni ukatili wa kiuchumi kwa wanaume wengi ndani ya familia.

Debora Mhekwa kutoka dawati la jinsia, amesema ukatili wa kiuchumi wanawake wamekuwa waathirika wakubwa haswa katika kipindi hiki cha mavuno ambapo mwenye sauti ya matumizi ya fedha ni baba tu lakini wakati kutafuta wamelima pamoja hali inayopelekea familia kupata ukatili wa kiuchumi.

Nao viongozi wa Dini wametoa wito kwa familia kuwekeza malezi yao juu ya hofu ya Mungu hili kuwa na familia bora na Taifa bora kwenye jamii.

Mchungaji Felix Mbogela amesema mzazi ukipata Mtoto wa kike jua sio wako bali unamuandaa kuwa mke wa mtu na ukipata Mtoto wa kiume jua sio wako bali unamuandaa kuwa mume wa mtu hivyo mzazi unapaswa kumulea Mtoto katika njia ya kumjua Mungu na kuwa na hofu ya Mungu.

"Tukiwalea watoto vizuri wenye hofu ya Mungu tutapata viongozi bora wa Taifa, tutapata watumishi bora serikalini hili Taifa la Tanzania liendelee kuwa bora"

Sheikh Yusuph Ally, amesema kila moja kwenye familia ni mchunga katika familia yake uwe mama, baba hivyo mwanaume hupaswi kufanya vitu pekee yako bila kushirikisha familia yako.

MWISHO.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.