• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

UPUNGUFU WA WATUMISHI WASABABISHA MRUNDIKANO WA KESI SONGWE

Posted on: July 7th, 2021

Upungufu wa watumishi katika Ofisi ya Mwendesha Mashtaka wa Serikali kwa Mkoa wa Songwe umepelekea mrundikano wa kesi hali inayoweza kusababisha ongezeko la uhalifu.

Mkuu wa Mkoa wa Songwe Mhe. Omary Tebweta Mgumba ameyasema hayo jana wakati akizungumza na Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Geofrey Mizengo Pinda alipofanya ziara ya siku mbili Mkoani hapa.

“Ofisi ya Mwendesha Mashtaka Mkoa wa Songwe inao watumishi wawili kati ya kumi wanaotakiwa kuwepo na hao wawili tu wanahudumia wilaya zote nne za Mkoa wetu, hawa lazima waelemewe na hivyo kupelekea kesi nyingi kuchelewa kukamilika, tunaomba mtutazame kwenye hilo.”, amesema  Mhe. Mgumba.

Ameongeza kuwa kuna changamoto ya ukosefu wa Mahakama za Wilaya ambapo kwa Mkoa wa Songwe ni Wilaya ya Mbozi pekee yenye mahakama huku Wilaya tatu zilizobaki zikitumia majengo ya kupangisha.

Mhe Mgumba pia amemueleza Naibu Waziri Pinda kuwa kuna ukosefu wa vifaa ikiwa ni pamoja na magari ambayo hutumika katika kusafirishia wafungwa pamoja na miundombinu ya maji katika magereza kutojitosheleza.

Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Geofrey Mizengo Pinda amesema kuhusu changamoto ya watumishi serikali imeendelea kutoa vibali vya ajira ili kuongeza idadi ya watumishi lakini Mkoa unapaswa kuangalia kesi ambazo sio za Msingi zifutwe ili kupunguza mrundikano wa kesi na mahabusu.

Naibu Waziri Pinda ameongeza kuwa kesi nyingine zinaingiza hasara serikali kwani zinakuwa hazina msingi lakini pia kwa kesi ndogondogo mahakimu waangalie namna ya kutoa vifungo vya nje ili kuipunguzia serikali mzigo wa kutunza wafungwa.

Pia amemsisitiza Mkuu wa Mkoa kuendelea kusimamia maadili ya mahakimu kwakuwa yeye ndiye Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ya Mahakama kwa ngazi ya Mkoa.

Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Geofrey Mizengo Pinda amefanya ziara ya Siku mbili mkoani Songwe ambapo ametembelea majengo ya mahakama, Mahabusu na Magereza.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.