• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

VIFAA VYA KUPAMBANA NA CORONA VYAGAWIWA SONGWE

Posted on: April 14th, 2020

Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imetoa vifaa mbalimbali vya kupambana na ugonjwa wa Virusi vya Corona kwa Mkoa wa Songwe huku ikiridhishwa na namna ambavyo Mkoa umechukua tahadhari dhidi ya ugonjwa huo.

Hayo yamebainishwa mapema leo na Mkuu wa Kitengo cha Maji Salama na Usafi wa Mazingira kutoka Wizara ya Afya Anyitike Mwakitalima wakati akikabidhi kwa Mkuu wa Mkoa wa Songwe vitakasa mikono lita 150, mashine za kutolea vitakasa mikono 30 na mashine mbili za kunawia bila kushika koki.

Mwakitalima amesema Wizara ya Afya inaendesha Kampeni ya Mikono Safi, Tanzania Salama ambapo pamoja na kutoa vifaa vya kupambana na ugonjwa wa virusi vya Corona kama vile vitakasa mikono pia hutoa elimu kwa wananchi namna ya kujikinga na Corona hasa kwa Mikoa iliyoko Mipakani kama Songwe.

Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brig. Jen. Nicodemus Mwangela ameipongeza Wizara ya Afya kwa kutoa vifaa hivyo hasa kwa Mkoa wa Songwe ambao upo Mpakani na ni Lango la kuingilia nchi za SADC ambapo vitakasa mikono 50 vinapelekwa katika jeshi la Polisi na 100 katika halmashauri zote.

Brig. Jen. Mwangela amesema,“Sisi Songwe ni Lango la SADC tukizubaa, tusipotoa elimu vizuri kwa Wananchi, tusipo chukua tahadhari ya kutosha tunaweza kuingiza Ugonjwa kutoka nchi jirani ambazo nazo zimeahirika na Corona”.

Ameongeza kuwa mpaka kufikia jana jumla ya wasafiri 180 wamewekwa karantini katika Halmashauri za Tunduma na Ileje  kwa muda wa siku 14 ikiwa ni jitihada za Serikali katika kuchukua tahadhari ya Ugonjwa wa Corona ambapo pia hakuna mshukiwa wa ugonjwa huo kwa Mkoa wa Songwe hadi sasa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe George Kyando ameishukuru Wizara ya Afya kwa kutoa kipaumbele kwa Jeshi hilo kwa kuwapatia vitakasa mikono kwakuwa wamekua wakisahaulika na wadau wengine huku akieleza kuwa anaendelea kutoa elimu kwa askari wachukue tahadhari zote muhimu wawapo katika majukumu yao.

Amesema katika mapambano dhidi ya Ugonjwa wa Corona Jeshi la Polisi lina mchango mkubwa katika kulinda karantini na maeneo waliyotengwa wagonjwa wa Corona, pia kukagua mabasi na magari yote ya abiria hivyo wako katika hatari ya kuambukizwa.

Balozi wa Kampeni ya Mikono Safi, Tanzania Salama Mrisho Mpoto maarufu kama Mjomba amesema vita ya kupambana na Ugonjwa wa Virusi vya Corona inahitaji ushirikiano wa wananchi wote waweze kunawa kwa maji tiririka na sabuni kila wakati bila kuchoka na kutoona kama adhabu.

Mpoto amesema wananchi wa Songwe wanapaswa kuacha mila za kusalimiana kwa kushikana mikono, kukumbatiana, kubusiana kuepuka misongamano isiyo ya lazima kwa kuwa mafanikio yatapatikana kwa umoja ikiwa wananchi wote watazingatia kauli mbiu ya Jilinde na Umlinde Mwenzio.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.