• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WADAU WATAKA KUONGEZWA KWA VITUO VYA KUGAWA MBOLEA ZA RUZUKU.

Posted on: September 22nd, 2022

WADAU WATAKA KUONGEZWA KWA VITUO VYA KUGAWA MBOLEA ZA RUZUKU.

SONGWE: Wadau wa kilimo Mkoani songwe wamewataka mawakala wa mbolea za ruzuku kuongeza idadi ya vituo ili kuwafikia wananchi wanaoishi maeneo ya vijijini.

Hayo yamesema wakati wa kikao cha kufungua msimu wa kilimo kwa mwaka 2022/23 kilicho fanyika Septemba 22 na kuhudhuriwa na makampuni ya mbolea, kampuni ya mbegu, maafisa kilimo, wakulima na Asasi za Kirai zinazojishughulisha na Kilimo.

Mkuu wa Wilaya ya Mbozi, Mhe. Cosmas Nshenye ambaye ni muwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Songwe amesema kitendo cha Mkulima wa Utambalila kufuata Mbolea ya Ruzuku umbali wa KM 70 atajikuta Mbolea amenunua kwa zaidi ya Bei ya Ruzuku ambayo Serikali imeweka.

Mhe. Cosmas Nshenye amewataka makala waliopewa kazi na Serikali ya kuuza Mbolea za Ruzuku kuongeza vituo zaidi karibu na wananchi ili kuwapunguzia mzigo.

"Mnaweza kuvitumia ata vyama vya ushirika ambayo viko karibu na wakulima kwa ajili ya kuuza Mbolea ya Ruzuku, kikubwa mawakala muangalie usalama wenu wa fedha" Mhe. Cosmas Nshenye.

Afisa Kilimo wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, Bi. Lydia Shonyela amewashauri mawakala kutumia maghala yaliyopo kwenye kila Kijiji kwa ajili ya kuuza Mbolea za Ruzuku ili kuwasaidia wakulima.

Julius Livingstone Afisa masoko wa kampuni ya ETG amesema Kampuni yao watajitahidi kuongeza na sehemu ambayo wakala watashindwa kufika kampuni itaona namna ya kumsaidia usafiri wakala lengo ni kuhakikisha Mbolea inawafikia wakulima wote kwa wakati.

Afisa Masoko Kampuni ya YARRA, Bi. Mwajuma Mwangu amesema ipo haja kwa makampuni ya mbolea kukaa pamoja kuhakikisha Bei ya Ruzuku kwa wateja wanaopatikana maeneo ya vijijini wapate Mbolea ya Ruzuku kwa bei sawa na mjini na kuepsha mkanganyiko kwa wananchi.

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Songwe, Ndg. Ellynico Mkola amesema vituo vingi vya mawakala vinapatikana mjini na kuwasahau wananchi wanao ishi maeneo ya vijijini ambako ndiko kuna maeneo makubwa ya kilimo.

Pia, Ndg. Mkola ametoa wito kwa wakulima wenzake kutumia vizuri fursa ya Mbolea ya Ruzuku kwa kuongeza tija kwenye mazao ili kuweza kumuunga mkono kwa vitendo Rais wa Tanzania, Mhe. Samia Suluh Hassan kwa kutoa Ruzuku ya Mbolea.

Mwenyekiti wa TCCA Mkoa wa Songwe, Ndg. Charles Chenza ametoa wito kwa wakulima kulima mazao zaidi ya moja ili kuweza kutumia vizuri fursa ya Mbolea ya Ruzuku.

Tunaishukuru sana Serikali ya awamu ya sita kwa kuweka Ruzuku ya Mbolea kwa mazao yote, tofauti na miaka ya nyuma Ruzuku ilikuwa inatolewa kwa zao la Mahindi tu, nawaomba wakulima wenzangu tulime mazao tofauti tofauti kwa kuwa Serikali imesikia Kilimo chetu na Ruzuku ipo kwa mazao yote.

Aidha, Mhe. Cosmas Nshenye amesema Mkoa wa Songwe utakuwa mwenyeji wa maadhimisho ya siku ya Mbolea Duniani itakayofanyika wilayani Mbozi kuanzia tarehe 11 hadi 13 Oktoba yatakayofunguliwa na Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Waziri Kindamba na kufungwa na Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe.

Serikali ya awamu ya sita imetenga fedha Bilioni 120 kwa ajili ya Mbolea ya Ruzuku ambayo imeanza kutolewa kwa mazo yote.

MWISHO.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.