• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

‘WAJASIRIAMALI ZINGATIENI UBORA WA BIDHAA MNAZOZALISHA ILI KUWALINDA WATUMIAJI’- RAS SONGWE.

Posted on: March 20th, 2018

  Wajasiriamali wadogo na wa kati wanaosindika vyakula Mkoani Songwe wamehimizwa kuzingatia ubora na usalama wa bidhaa wanazozalisha ili kulinda afya za wanaotumia bidhaa zao.

Rai hiyo imetolewa mapema leo na Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Songwe Herman Tesha wakati akifungua mafunzo ya siku mbili ya wajasiriamali wanaosindika vyakula mkoani hapa yaliyoandaliwa na Mamlaka ya Chakula na Dawa Nchini (TFDA).

Tesha amesema, kuelekea uchumi wa viwanda wasindikaji hao wanapaswa kuzingatia sheria na taratibu pamoja na matumizi ya teknolojia mpya na za kisasa zaidi katika kusindika bidhaa zao ili ziweze kushindana katika soko kitaifa na mataifa.

“Teknolojia inakua na mawasiliano yamerahisishwa, wasindikaji msibweteke hakikisheni bidhaa zenu ni bora ili kwanza muweze kulinda afya za watumiaji pili muweze kushindana na kuliteka soko la kitaifa na kimataifa”, amesisitiza Tesha.

Aidha amewataka wajasiriamali hao kuwa mabalozi wazuri wa elimu waliyoipata kwa wananchi wengine na wajasiriamali wengine kutokana na kuwa mkoa wa Songwe una pakana na nchi jirani na hivyo kuwa na uwezekano wa kupitishwa bidhaa zisizo halali.

“Sisi tuko mpakani, vipodozi haramu na vyakula visivyo faa vinaweza kuzagaa katika maeneo yetu, hivyo basi elimu hii tunayoipata katika mafunzo haya hasa ya kutambua bidhaa halali na bandia itusaidie kuwa mabalozi wazuri pamoja na sisi wenyewe kuhakikisha bidhaa zetu ni halali”, ameongeza.

Tesha amewataka wajasiriamali hao kutosubiri kuletewa mafunzo bali pale wanapoona kuna uhitaji wazifuate taasisi husika ili ziwape elimu hiyo huku akisisitiza kuwa taasisi hizo pia zina wajibu wa kuwasaidia wajasiriamali kwa kuwapa mafunzo na elimu.

Kaimu Mkurugenzi wa Usalama wa Chakula kutoka TFDA Justin Makisi ameeleza kuwa idadi kubwa ya wajasiriamali wamekuwa wakiendesha shughuli zao bila kujua wala kufuata sheria na taratibu.

Makisi ameeleza kuwa wajasiriamali hao hasa wasindikaji wa vyakula wadogo na wa kati hawajasajili bidhaa zao kutokana na kushindwa kumudu gharama za uchunguzi wa maabara wa bidhaa zao ili ziweze kusajiliwa huku wengine wakiwa hawafahamu endapo wanatakiwa kusajili bidhaa zao.

Naye Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Songwe Dkt. Kheri Kagya amewataka wajasiriamali hao kufuatilia mafunzo hayo kwa umakini kwakuwa yatawasaidia katika ushindani wa bidhaa zao kwenye soko la kimataifa.

Dkt Kagya amewaeleza wasindikaji hao kuwa ubora na usalama wa bidhaa zao ni kigezo mojawapo katika kuliteka soko la kimataifa na hivyo kukuza uchumi wa taifa.

Kwa upande wao wajasiriamali wasindikaji wa vyakula mkoani Songwe wameeleza kuwa changamoto walizonazo katika utekelezaji wa shughuli zao ni pamoja na majengo ya kusindikia bidhaa zao kutokidhi vigezo vya TFDA pamoja na uhaba wa vifungashio bora vya bidhaa zao.

Wajasiriamali wanaosindika vyakula mkoani Songwe wakishiriki mafunzo ya siku mbili yaliyoandaliwa na Mamlaka ya Chakula na Dawa Nchini (TFDA).


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.