• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WANAFUNZI SONGWE KUPANDA MLIMA KILIMANJARO

Posted on: August 31st, 2019

  Wanafunzi wawili kutoka Wilayani Songwe wanatarajiwa kupewa nafasi ya Kupanda Mlima Kilimanjaro mwezi ujao ikiwa ni sehemu ya Kumbukumbu ya Miaka 20 ya Kifo cha baba Taifa hayati J. K. Nyerere itakayofanyika Oktoba 14 mwaka huu Mkoani Lindi.

Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brig. Jen. Nicodemus Mwangela ametoa ahadi hiyo mapema leo wakati wa mazoezi ya viungo na Uzinduzi wa Club ya Mkwajuni Jogging club ya Wilayani Songwe.

Kabla ya uzinduzi huo, Brig. Jen. Mwangela amewaongoza wananchi wa Wilaya ya Songwe kufanya mazoezi ya kukimbia yaani Jogging kwa takribani kilomita saba pamoja na kufanya mazoezi mbalimbali ya viungo.

Aidha amesema Mkoa wa Songwe tayari una jumla ya vijana 11 ambao wameshapanda Mlima Kilimajaro kama sehemu ya kuonyesha uzalendo wao na vijana hao ni wale ambao hupenda kufanya mazoezi.

“Wanafunzi fanyeni mazoezi kwa ajili ya afya ya mwili na akili pia tutachagua wanafunzi wawili ambao watapewa mazoezi na wana Kimondo Jogging Club, mazoezi hayo yanahusisha kupanda Mlima Rungwe angalau mara mbili ndipo muweze kupanda Mlima Kilimanjaro, nitajitahidi tupate wanafunzi wa kike na wa kiume mtuwakilishe”, Bri. Jen. Mwangela

Amesisitiza kuwa mazoezi ni mazuri kwa afya na ni ajira, pia amewapongeza wananchi wa Waliojitokeza kushiriki mazoezi hayo huku akiwasisitiza kuendeleza utaratibu wa kufanya mazoezi mara kwa mara.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Songwe Dkt Kheri Kagya amesema kila mtu anapaswa kufanya mazoezi angalau kwa muda wa dakika 30 kila siku ili kujiepusha na magonjwa yasiyoambukiza ambayo kwa sasa husababisha vifo kwa zaidi ya asilimia 30.

Dkt Kagya amesema kufanya mazoezi huondoa mafuta yasiyotakiwa mwilini, husaidia mzunguko wa damu kufanya kazi vizuri na ukifanya mazoezi kwa muendelezo mwili utaweza kuepuka magonjwa ya mara kwa mara.

Bi Shuhudia Huseni Musa mkazi wa Mkwajuni Wilayani Songwe amesema amefurahia kufanya mazoezi  licha kupata maumivu ya viungo kwakuwa ilikuwa ni mara yake ya kwanza kufanya mazoezi kama hayo.

Amesema kwa kufanya mazoezi kila siku kunaweza kusaidia kujikinga na magonjwa kama vile shinikizo la damu, kisukari, uzito uliozidi hivyo anawashauri watu wazima hususani wanawake wawe na tabia ya kufanya mazoezi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.