• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WANANCHI WAANDALIWE VIZURI KUPOKEA MRADI, RC KINDAMBA.

Posted on: October 27th, 2022

WANANCHI WAANDALIWE VIZURI KUPOKEA MRADI, RC KINDAMBA.

MBOZI: Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Waziri Kindamba amemuagiza Mkuu wa wilaya ya Mbozi na Mkurugenzi kuanza kuwaandaa wananchi wa Kijiji cha Iboya kilichopo Kata ya Ihanda kwa ajili kupokea mradi wa mkubwa wa kituo cha kimataifa cha ukaguzi wa magari yanayofanya safari za nje ya Nchi.

Amesema hayo Oktoba 25, wakati akiongea na wananchi wa Iboya eneo ambalo mradi unatarajiwa kujengwa, Serikali ya awamu ya sita ni ya vitendo na inayokwenda kwa kasi katika kutekeleza miradi.

Mhe. Waziri Kindamba amewatoa hofu wananchi juu utekelezaji wa mradi na ametolea mfano wa Barabara ya TANZAM kutoka Tunduma hadi Mbeya kwa muda mrefu imekuwa ikisemwa itajengwa kwa njia 4 lakini chini ya Mhe. Samia Suluhu Hassan sasa inakwenda kujengwa na hii ndio maana halisi ya Kazi inaendelea.

"Mjiandae na fedha ambazo mtapata za fidia kwa ajili ya kuboresha uchumi wa familia zenu, mjiandae na shughuli za kiuchumi ambazo zitakuwa zinafanyika hapa wakati wa utekelezaji wa mradi na baada ya mradi kukamilika" Mhe. Waziri Kindamba.

Mwananchi unaweza kupata milioni 30 za fidia alafu wewe hujawai shika ata milioni, sasa kama hujajiandaa utakuta unachanganikiwa, viongozi mfike hapa muanze kuwaanda wananchi na kuwapa elimu ya fedha amesema Mhe. Waziri Kindamba.

Pia, Mhe. Waziri Kindamba ameitaka TANROADS baada kukamilisha tathinini wawalipe fedha wananchi ili waendelee na maisha mengine.

Kaimu Meneja wa TANROADS Songwe, Mhandisi, Suleiman Bishanga amesema kituo kitakuwa na ukubwa wa umbali wa KM 2 kwa pande zote za Barabara na itachukua mita 300 kila upande wa Barabara.

"Miundombinu itakayojengwa ni Hoteli, maegesho ya magari, mizani ni eneo ambalo litakuwa kiuchumi na wasafirishaji na wasafiri watapumzika" Mhandisi Bishanga.

Meneja wa TANROADS amesema uthaminishaji uanaanza upya, na wiki ijayo kamati za uthaminishaji za kijiji zitaundwa.

Mkazi wa Iboya, Bi. Sister Mwakyusa ameiomba Serikali kufanya haraka kwa tathimini na kuwalipa, wasicheleweshe kama awali walikaa zaidi ya miaka 3 bila kujua kinachoendelea ila kwa kuwa leo mumekuja viongozi wakubwa basi tunaomba mtusaidie jambo likamilike haraka.

MWISHO.

 

 

 

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.