• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WANANCHI WANUFAIKA NA AJIRA KWENYE MIRADI YA MAJI.

Posted on: September 1st, 2022

WANANCHI WANUFAIKA NA AJIRA KWENYE MIRADI YA MAJI.

MBOZI: Wananchi waliopata ajira kwenye miradi ya maji inayotekelezwa na Wakala wa maji na usafi wa mazingira vijijini (RUWASA) Wilaya ya Mbozi wameishukuru Serikali kwa kuleta miradi ya maji iliyopelekea wapate kazi kwenye miradi hiyo.

Wananchi wameonyesha furaha hiyo wakiwa wanaendelea na kazi katika mradi wa maji wa Old Vwawa ambao uko hatua za ukamilishaji ili uanze kutoa maji safi na salama kwa ajili ya wananchi wapatao elfu 3 wanaoishi Old Vwawa.

Keston Mwashiuya fundi aliyepata kazi ya ujenzi katika mradi wa Old Vwawa amesema ajira zinazotolewa na RUWASA ni nzuri, wanalipa vizuri na ameiomba Serikali kuendelea kuleta miradi ya maji wilaya ya Mbozi ili wazidi kunufaika na kukuza uchumi wa familia zao.

“Sisi wananchi wa hali ya chini miradi hii mbali ya kutuletea maji safi na salama lakini inatusaidia sana kwa kutupatia ajira na maisha yetu yanaendelea vizuri” Keston Mwashiuya.

Elia Nzunda ameiomba RUWASA kuendelea kuwaamini katika kazi mbalimbali na wao watafanya kazi za ubora na thamani kama wanavyohitaji RUWASA kwani kwa takribani miaka 3 nimefanya kazi za ufundi katika miradi mbalimbali inayotekelezwa na RUWASA wilaya ya Mbozi na nimeona tofauti na kazi ambazo alikuwa anafanya sehemu nyingine.

Meneja wa RUWASA Wilaya ya Mbozi, Mhandisi Gratius Haule amesema kwa makadirio mradi moja wa maji unatoa ajira za mafundi wapatao 20 kwa ujenzi wa nyumba ya pampu na tenki la kuhifadhia maji, wananchi kati ya 100 na 200 wanapata ajira za kuchimba mitaro ya kulaza mabomba za maji na kupelekea mradi moja kuajiri watu zaidi ya 200.

“Naishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa sasa Wilaya ya Mbozi katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali inampango wa kujenga miradi 6 kwa shilingi Bilioni 5 kwenye vijiji mbalimbali ambavyo havina huduma ya maji safi na salama, tunategemea tutazalisha ajira nyingine nyingi katika miradi hii” Mhandisi Gratius Haule.

Meneja wa RUWASA Wilaya ya Mbozi, Mhandisi Gratius Haule amesema Serikali ya awamu ya sita chini ya Mhe. Samia Suluh Hassan Rais wa Tanzania imepanga ifikapo 2025 vijiji vyote ndani ya wilaya ya Mbozi viwe na maji safi na salama na ujenzi wa miradi utaendelea kila mwaka.

Wakati RUWASA inaanzishwa 2019 upatikanaji wa maji katika wilaya ya Mbozi ulikuwa asilimia 46 lakini hadi 2022 upatikanaji wa maji kwa sasa umeongezeka na kufika asilimia 73 zote izi juhudi kubwa ambazo zimefanywa na Serikali, lengo ifikapo 2025 maji vijijini yapatikane kwa zaidi ya asilimia 100.

MWISHO.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.