• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WANAOFANYA MIZAHA YA CORONA KUCHUKULIWA HATUA

Posted on: March 22nd, 2020

Imebainika kuwa wapo baadhi ya watu ambao hutumia mitandao ya kijamii kutengeneza na kusambaza mizaha na taarifa za uongo juu ya Ugonjwa wa Virusi vya Corona huku wakiwaaminisha wengine kuwa ugonjwa huo hauwapati watu weusi.

Akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Songwe katika Kikao cha Kutathmini utayari wa Kupambana na Ugonjwa wa Corona Endapo utatokea Mkoani Songwe, Mkuu wa Wilaya ya Mbozi John Palingo amesema watu hao watachukuliwa hatua kali.

Palingo amesema mizaha hiyo inadhoofisha mapambano dhidi ya Ugonjwa wa Corona na kuwafanya wananchi wengine kutotilia maanani maelekezo ya wataalamu wa Afya ya kuchukua hatua za tahadhari kwakuwa mapambano hayo ni vita ambayo inajumuisha jamii nzima.

Amesema kuwa licha ya Mamlaka ya Mawasiliano Nchini (TCRA) kutangaza kuwachukulia hatua kali wote wanao sambaza mizaha na taarifa za uongo kuhusu Ugonjwa wa Corona, Uongozi wa Mkoa wa Songwe na Wilaya zote pia hauta wavumilia wote watakaofanya vitendo hivyo Mkoani hapa.

Palingo ameongeza kuwa wazazi na walezi wote wahakikishe wana waangalia watoto wote wasizagae mitaani, sokoni, minadani na katika mikusanyiko ya masomo ya ziada (Tuisheni) kwani serikali imefunga shule ili kuchukua tahadhari ya kuwakinga wanafunzi dhidi ya Ugonjwa wa Corona.

Amesema serikali inaendelea kusisitiza Sehemu ambazo lazima mikusanyiko iwepo kama katika nyumba za ibada na katika ofisi mbalimba, maji ya kunawa na sabuni yawepo na pia hatua zote muhimu za tahadhari zichukuliwe.

Aidha Palingo amewataka wananchi wa Mkoa wa Songwe kuacha masuala ya mila yanayoweza kuwawaweka katika hatari ya kuambukizana ugonjwa wa Corona hususani mila ya kusalimiana kwa kushikana mikono.

Amesema waanchi wanapaswa kuelewe kuwa wasisubiri ifikie hatua ya kutibu wagonjwa wa corona bali wazuie Kwanza kwa kuchukua tahadhari ya kujikinga kwani ikifikia hatua ya kutibu watu wengi wanaweza kupoteza maisha.

Naye Mganga Mkuu wa Mkoa wa Songwe Dkt Hamadi Nyembea amesema Mkoa wa Songwe unatoa elimu ya kujikinga na ugonjwa wa Corona kwa wananchi kwa ngazi zote kwani ni njia mojawapo ya kupambana na ugonjwa huo.

Dkt Nyembea amesema Kamati za Afya za Wilaya hadi ngazi ya Kata zitahakikisha zinafikisha elimu ya kujikinga na Corona kwa wananchi pia maafisa wengine wa Serikali nao washiriki kuwaelimisha wananchi.

Sauli Ndambo Mkazi wa Ilembo Wilaya ya Mbozi ameishukuru serikali kwa kuchukua tahadhari na kufunga shule ili watoto wawe salama huku akiwataka wanao fanya mizaha kuacha mara moja kwani ugonjwa huo hauna mzaha na unaua.

Laurent Mwasile Mkazi wa Vwawa Wilaya ya Mbozi amewasihi vijana kuchukua tahadhari na kuacha mila ya kusalimiana kwa mikono na endapo watamuona mtu mwenye dalili za ugonjwa huo watoe taarifa katika vituo vya Afya.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.