• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WANAWAKE WANA FURSA KUBWA KUELEKEA UCHUMI WA VIWANDA-RC SONGWE.

Posted on: March 8th, 2018

  Kuelekea Tanzania ya Viwanda wanawake hususani wa Mkoa wa Songwe wameelezwa kuwa wanayo fursa kubwa katika kuanzisha viwanda vipya na kusaidia kufufua viwanda vilivyopo kwa kupeleka bidhaa zao katika viwanda hivyo.

Mkuu wa Mkoa wa Songwe Chiku Gallawa ameeleza hayo mapema leo katika viwanja vya shule ya Msingi Tunduma katika maadhimisho ya Siku ya wanawake Duniani huku akisisitiza kuwa wanawake sasa wajikite katika kuanzisha viwanda.

 “Mwanamke amekuwa mzalishaji mkubwa wa mazao ya shambani, ameweza kuongeza thamani ya mazao yake pamoja na shughuli nyingine za uzalishaji mali, tunapoelekea kwenye uchumi wa viwanda hii ni fursa kubwa kwakuwa sasa tunatakiwa kuanzisha viwanda na tayari malighafi tunazo za kutosha”, amesema Gallawa.

Ameongeza kuwa wanawake wanapoendelea kuzalisha mali wajikite sasa katika kuboresha bidhaa zao ili ziweze kupata soko na kukubalika katika viwanda na masoko pamoja na kujiunga kwenye vikundi ili kupata urahisi wa mikopo.

Aidha Gallawa ameziagiza halmashauri zote Mkoani Songwe kuhakikisha wanatoa mikopo kwa vikundi vya wanawake, ambayo itawasaidia kununua mashine na malighafi kwa ajili ya kuanzisha kiwanda huku akisisitiza mkopo kwa kikundi kimoja usipungue shilingi milioni 20.

“Kwa mkoa mzima wa Songwe tulitenga bilioni 1.2 kwa ajili ya wanawake, vijana na walemavu sasa naagiza halmashauri zote hakikisheni mnavipa vikundi vyenu mikopo, angalau isipungue milioni 20 na sio kuwapa fedha kidogo ambazo haziwanui kiuchumi’’, amesisitiza Gallawa.

Gallawa amezitaka halmashauri kusimamia vikundi hivyo kwa kuwatoa wataalamu kama maafisa biashara, vijana, ushirika na maendeleo ya jamii ili kuviandalia vikundi maandiko ya miradi yao na ushauri wa kitaalamu wa uendeshaji wa vikundi vyao.

“Jukumu la halmashauri ni kulea vikundi vyote, sio mkiwapa mkopo mnawatelekeza, mnatakiwa kuvisaidia kuandaa andiko la mradi, hii sio huruma au hisani ni wajibu wenu”, amefafanua Gallawa.

Gallawa amewasihi pia wanawake kugombea nafasi za uongozi kuanzia ngazi ya serikali za vijiji ili wawe watetezi wa wanawake akitoa mfano kuwa kati ya vijiji 307 vya mkoa wa Songwe ni kijiji kimoja tu ndio kuna mwenyekiti wa kijiji mwanamke.

Nao wanawake waliojitokeza katika maadhimisho hayo wamemueleza Mkuu wa Mkoa changamoto za kukosa mikopo na elimu zaidi ya ujasiriamali ili waweze kujikwamua kiuchumi.


  Mwanamke mkazi wa Tunduma akionyesha kuwa wanawake wanaweza kufanya kazi yoyote kwa kumsaidia fundi aliyekuwa akijenga katika kituo cha afya cha Tunduma.

Mkuu wa Mkoa wa Songwe Chiku Gallawa akizungumza na mgonjwa katika kituo cha afya Tunduma alipowatembelea wagonjwa na kuwafariji kama sehemu ya maadhimisho ya siku ya wanawake duniani mapema leo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.