• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WATOTO 287,512 KUPATIWA CHANJO YA POLIO

Posted on: August 30th, 2022

WATOTO 287,512 KUPATIWA CHANJO YA POLIO

SONGWE:  Serikali mkoani Songwe imedhamilia kuwafikia watoto 287,512 wenye umri chini ya miaka 5 na kuwapatia chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa Polio katika kampeni itakayofanyika kwa siku Nne kuanzia tarehe 1 mpaka tarehe 4 mwezi Septemba.

Hayo amesema mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Songwe Mhe. Cosmas Nshenye ambaye ni mkuu wa wilaya ya Mbozi katika kikao cha afya ya msingi ngazi ya Mkoa kilichofanyika leo Agosti 30 na kujadili mikakati ya utekelezaji wa Kampeni ya Polio.

Mhe. Cosmas Nshenye amesema kampeni hii ya Polio watalamu watapita nyumba kwa nyumba na maeneo yote yenye watoto wenye umri chini ya miaka mitano pamoja na vituo vya kutolea huduma za Afya  ili kufikia malengo ya kuwakinga watoto wote dhidi ya ugonjwa hatari wa Polio.

Muwakilishi wa Mkuu wa Mkoa, Mhe. Cosmas Nshenye ametoa wito kwa wazazi/walezi wenye watoto wa umri chini ya miaka 5 kuhakikisha mtoto anapata chanjo ya matone ya Polio kwani Mtoto asiyepata chanjo Ni hatari kwa maisha yake na kwa jamii inayomzunguka.

Mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani Dkt. Robert Hongo amesema kwa sasa Tanzania haina ugonjwa huu ila inachukua hatua usiingie nchini tangu utangazwe mwezi Januari 2022 nchini Malawi na Msumbuji ambazo ziko jirani na Tanzania na ukizingatia mwingiliano wa watu ni mkubwa hivyo hatua stahili za kuwakinga watoto kwa chanjo ya matone ya Polio ni muhimu.

Katibu Tawala Mkoa wa Songwe, Bi. Happiness Seneda amesema ni vyema jamii ikajua athari za ungonjwa Polio kwa upana wake ili waweze kujitokeza kwa wingi kuwapatia chanjo watoto wao.

"Baada ya Nchi kutoa chanjo ugonjwa huu ulipotea sasa watu wengi wanausikia tu, ni vyema jamii ikapata athari za ugonjwaa huu kwa undani" Bi. Happiness Seneda.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Dkt. Boniface Kasululu amesema katika Kampeni hii ya chanjo ya Polio inayoanza tarehe 1 Septemba watoto wote wenye umri chini ya miaka mitano watapata chanjo hata kama ametoka kupata chanjo hiyo siku moja kabla.

Pia, Dkt. Kasululu amesema ata kama Mtoto alipata chanjo ya matone kwa ratiba yake ya kliniki lakini ndani ya siku nne za kampeni hii Mtoto huyo atapata chanjo tena.

Mratibu wa Chanjo Mkoa wa Songwe, Bwn. Moses Lyimo amesema wamejipanga vizuri kuhakikisha kampeni inafanyika vizuri na kuwafikia watoto lengwa wote pamoja na kutoa elimu kwa wazazi/walezi kupitia vyombo vya Habari juu ya athari ya ugonjwa wa Polio kwenye jamii.

Kampeni hii ya Polio ni ya nne tangu kutangazwa kwa ugonjwa wa Polio Nchini Malawi lengo kuchukua hatua ya kujikinga dhidi ya ugonjwa huu hatari wa Polio.

MWISHO.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.