• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WAZIRI UMMY ARIDHISHWA NA UTENDAJI WA SEKTA YA AFYA MKOA WA SONGWE.

Posted on: March 7th, 2018

  Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu amefanya ziara ya siku mbili Mkoani Songwe katika Wilaya za Mbozi na Ileje na kuridhishwa na mafanikio ya sekta ya  Afya Mkoani hapa.

Waziri Ummy ambaye amehitimisha ziara yake leo amesema Songwe inafanya vizuri katika sekta ya afya licha ya kuwa na upungufu wa watumishi na baadhi ya miundombinu.

“Songwe mna upungufu wa watumishi takriban asilimia sitini lakini mmefanya vizuri, hii inaonyesha jinsi ambavyo watumishi wa sekta ya afya mkoani hapa wanajitoa kuihudumia jamii”, amesema.

Ameongeza kuwa Songwe imeweza kupunguza vifo vya akina mama wajawazito huku asilimia ya akina mama wanaojifungulia katika vituo vya kutolea huduma za afya ikiongezeka, hii ni ishara tosha kuwa huduma za afya sasa zimeboreka.

“Nimeona kwa mfano Wilaya ya Mbozi kati ya akina mama 12995 waliojfungua sita tu ndio waliopotea maisha, mmejitahidi sana  na hongereni pia natamani mikoa mingine ijifunze Songwe hasa katika matumizi ya njia za kisasa za uzazi wa mpango ambavyo zinaweza kupunguza vifo vya akina mama wajawazito”, amefafanua Waziri Ummy.

Ameeleza kuwa Wizara ya Afya itatangaza ajira hivi karibuni na kuahidi kuwa Songwe itapatiwa watumishi kwakuwa iko kati ya mikoa tisa itakayopewa kipaumbele huku akiwataka wakurugenzi wa halmashauri zote nchini kujiandaa kuwapokea watumishi hao ili waweze kubaki katika vituo walivyopangiwa.

Aidha katika ziara yake Wilayani Ileje katika kata ya Lubanda Waziri Ummy aliweza kushuhudia adha ya miundombinu ya barabara kutopitika kwa urahisi na kuishauri Wakala wa Barabara za Vijijini (TARURA) kushughulikia barabara hiyo ili ipitike kwa urahisi na hivyo kuokoa maisha ya akina mama wajawazito na wagonjwa wengine.

Nao akina mama waliojitokeza katika zahanati ya Lubanda wamemshukuru Waziri Ummy na serikali ya awamu ya tano kwa kuwapatia milioni mia tano zitakazowezesha ujenzi wa chumba cha upasuaji, maabara ya damu, nyumba ya daktari na chumba cha kuhifadhia maiti.

Akina mama hao wamesema adha kubwa waliyokuwa wakiipata hasa ya kusafiri umbali mrefu kwa ajili ya kupata huduma za upasuaji wa mama na mtoto sasa zitakwisha.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Songwe Chiku Gallawa amemuhakikishia Waziri Ummy kuwa Mkoa utaendelea kusimamia na kutekeleza kwa ufanisi shughuli na maelekezo yote ya serikali yanayohusu Sekta ya afya ili kuiboresha zaidi sekta hiyo.

  Wanakijiji cha Mtura Kata ya Lubanda Wilayani Ileje wakizungumza na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu alipofanya ziara kijijini hapo kujionea maendeleo ya ujenzi katika kituo cha Afya cha Lubanda.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.